Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19 ilitukuta bila kujiandaa, lakini tumejifunza-Wananchi Kenya
Maadhimisho ya miaka 75 wa Umoja wa Mataifa yanafanyika wakati dunia inakabiliwa na janga baya zaidi kuwahi kushuhudiwa kwa miaka mingi, virusi vya corona. Vifo pamoja na hasara nyingine kama kupoteza kazi na biashara, vimerudisha nyuma maendeleo yaliyofikiwa kwa miongo mingi. Lakini watu wameweza kujifunza nini hasa kutokana na janga hili la virusi vya corona? Mwandishi wetu wa Kenya Jason Nyakundi amezungumza na baadhi ya wananchi wa Kenya.
Lugha ya ishara lazima ijumuishwe katika kujikwamua na janga la COVID-19
Mwaka huu siku ya kimataifa ya lugha ya ishara inaadhimishwa katikati ya janga la corona au COVID-19, janga ambalo limemkumba kila mtu wakiwemo jamii ya viziwi, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Siri ya Tanzania katika kuidhibiti COVID-19
Wakati hii leo, wakuu wa nchi na wawakilishi wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanashiriki mkutano wa ngazi ya juu wa UNGA75 wa kujadili jinsi ya kuepusha upotoshaji wa taarifa na usambazaji wa taarifa potofu wakati huu wa janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19, Tanzania imetaja siri ya mafanikio yake katika kudhibiti gonjwa hilo mara baada ya kubainika mwezi Machi mwaka huu. Flora Nducha na maelezo zaidi.
Tanzania haikuongozwa na mihemuko ya kisiasa katika kukabili COVID-19 – Balozi Gastorn
Wakati hii leo, wakuu wa nchi na wawakilishi wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanashiriki mkutano wa ngazi ya juu wa UNGA75 wa kujadili jinsi ya kuepusha upotoshaji wa taarifa na usambazaji wa taarifa potofu wakati huu wa janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19, Tanzania imetaja siri ya mafanikio yake katika kudhibiti gonjwa hilo mara baada ya kubainika mwezi Machi mwaka huu.
Tuimarishe mshikamano vita dhidi ya COVID-19 na tukomeshe hewa ukaa ifikapo 2060: China
Rais wa Uchina Xi Jinping ametoa wito wa mshikamano wa kimataifa kupambana na virusi vya corona wakati wa hotuba yake hii leo kwenye mjadala wa Baraza Kuu akidai kwamba nchi yake inalenga kuwa huru bila hewa ukaa katika vita kubwa dhidi ya mabadiliko ya tabianchi ifikapo mwaka 2060.
Miaka 75 tumepiga hatua kubwa na tuna ya kujivunia, lakini safari bado ni ndefu:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema Umoja wa Mataifa una mengi ya kujivunia baada ya kupiga hatua kubwa tangu kuanzishwa kwake miaka 75 iliyopita, lakini bado safari ni ndefu inayohitaji mshikamano wa kimataifa na utashi wa hali ya juu wa kisiasa kukabili changamoto zinazokikikumba kizazi hiki na vijavyo.Jason Nyakundi na maelezo zaidi.
Tukio la SDGs laadhimishwa kwa mara ya kwanza
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo amefungua tukio la Malengo ya maendeleo endelevu, SDG jijini New York Marekani ambalo litakuwa linafanyika kila mwaka katika miaka hii kumi ya kuelekea kutimiza malengo hayo ifikapo mwaka 2030. Bwana Guterres ameuambia ulimwengu kupitia mkutano hio kuwa tukio hili la kujadili masuala ya malengo endelevu ni fursa kuonesha kuwa kama familia moja ya mataifa iliyoungana, “tuna kila kinachotakiwa ili kutokomeza umaskini na njaa, kudhibiti mabadiliko ya tabianchi, kufikia usawa wa kijinsia na kufanikisha malengo 17 ya kimataifa.”
Ripoti imebaini watoto milioni 150 zaidi wametumbukia katika umaskini kwa sababu ya COVID-19-
Idadi ya watoto wanaoishi katika umaskini wa namna mbalimbali imeongezeka hadi takriban bilioni 1.2 kutokana na janga la COVID-19. Hiyo ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na shirika la Save the Children uliochapishwa hii leo mjini New York Marekani na London Uingereza. Jason Nyakundi na maelezo zaidi.
Watoto milioni 150 zaidi wametumbukia katika umaskini kwa sababu ya COVID-19-Ripoti
Idadi ya watoto wanaoishi katika umaskini wa namna mbalimbali imeongezeka hadi takriban bilioni 1.2 kutokana na janga la COVID-19. Hiyo ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na shirika la Save the Children uliochapishwa hii leo mjini New York Marekani na London Uingereza.
COVID-19 imenirudisha nyumbani kijijini-Waweru
Tangu lizuke janga la corona duniani athari nyingi za karibu kila sekta zimeshuhudiwa. Vijana ambao idadi yao ndiyo kubwa kwa karibu kila nchini duniani nao wameathirika pakubwa. Wengi walilazimika kusitisha masomo kufuatia kufungwa shule na taasisi za elimu, wengine wakapoteza ajira na kubaki katika hali ya sintofahamu kuhusu hatma ya maisha yao. Kijana Joseph Waweru alipoteza kibarua chake mjini Nairobi na pia mipango yake ya masomo katika chuo kikuu ikakwama ndipo akaamua kuhamia kwao alikozaliwa huko Kitale, magharibi mwa Kenya.