Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Kijana Tanzania atengeneza ndoo ya kunawa mikono bila kugusa koki wala sabuni.
UN News/ UNIC Tanzania

COVID-19: Kijana Tanzania atengeneza ndoo ya kunawa mikono bila kugusa koki wala sabuni

Ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 ukiwa umeshasambaa katika mataifa 199 ikiwemo Tanzania, vijana nao wanaibuka na ubunifu mbalimbali ili kusaidia mataifa yao katika kudhibiti kuenea kwa gonjwa hilo lisilo na tiba wala chanjo. Ubunifu wa vifaa vya kudhibiti kuenea umefanywa na kijana mmoja nchini Tanzania kama anavyoripoti… wa kituo cha habari za Umoja wa Mataifa, UNIC jijini Dar es salaam.

Sauti
2'

30 Machi 2020

Assumpta Massoi : Hujambo na Karibu kusikiliza Jarida kutoka Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa, kutoka hapa New York Marekani.

JINGLE (04”)      

ASSUMPTA:Ni Jumatatu ya Machi 30 mwaka 2020, mwenyeji wako studioni hii leo ni mimi ASSUMPTA MASSOI 

Sauti
11'22"
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Tijjani Muhammad-Bande ashiriki mkutano kwa njia ya mtandao wa wanachama wa UN kuhusu virusi vya corona.
United Nations/Reem Abaza

UN yawajulisha nchi wanachama kuhusu mapambano dhidi ya COVID-19

Katika mkutano maalum kupitia njia ya mtandao uliofanyika leo Katibu Mkuu wa moja wa Mataifa, Rais wa Baraza Kuu la Umoja huo, Baraza la Usalama na baraza la kiuchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC wamezijulisha nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhusu juhudi za Umoja huo katika kupambana na virusi vipya vya Corona, COVID-19 na kuendelea na kazi muhimu ya shirika hilo duniani kote.

WFP/Challiss McDonough

Mlipuko wa COVID-19 unaathiri uwasilishaji wa mlo shuleni-WFP

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP leo limezindua ramani mpya ya kidijitali inayodhihirisha athari za virusi vya Corona, COVID-19 katika program zake za mlo mashuleni. Flora Nduicha na taarifa kamili

(TAARIFA YA FLORA NDUCHA)

Kwa mujibu wa WFP ramani hiyo ambayo ni ya “ufuatiliaji wa kimataifa wa mlo mashuleni wakati wa kufungwa shule kutokana na mlipuko wa COVID-19 inatoa inatoa maenedeleo mapya ya kila siku kuhusu kufungwa kwa shule na idadi ya Watoto ambao hawapati tena mlo mashuleni kutokana na janga hili la Corona.

Sauti
1'15"