Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19: Kijana Tanzania atengeneza ndoo ya kunawa mikono bila kugusa koki wala sabuni
Ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 ukiwa umeshasambaa katika mataifa 199 ikiwemo Tanzania, vijana nao wanaibuka na ubunifu mbalimbali ili kusaidia mataifa yao katika kudhibiti kuenea kwa gonjwa hilo lisilo na tiba wala chanjo. Ubunifu wa vifaa vya kudhibiti kuenea umefanywa na kijana mmoja nchini Tanzania kama anavyoripoti… wa kituo cha habari za Umoja wa Mataifa, UNIC jijini Dar es salaam.
30 Machi 2020
Assumpta Massoi : Hujambo na Karibu kusikiliza Jarida kutoka Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa, kutoka hapa New York Marekani.
JINGLE (04”)
ASSUMPTA:Ni Jumatatu ya Machi 30 mwaka 2020, mwenyeji wako studioni hii leo ni mimi ASSUMPTA MASSOI
Waajiri saidieni familia za wafanyakazi wakati huu wa COVID-19 – ILO/UNICEF
Mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa, lile la kuhudumia watoto, UNICEF na lile la kazi, ILO leo wametoa mapendekezo ya jinsi waajiri wanaweza kusaidia waajiriwa na familia zao wakati huu wa janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19.
Janga la COVID-19 latishia kusambaratisha afya na uchumi katika nchi zinazoendelea:UNDP
Taarifa iliyotolewa leo na shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP imeonya kwamba kusambaa kwa virusi vya Corona, COVID-19 kunatishia kusambaratisha nchi zinazoendelea sio katika mgogoro wa kiafya pekee wa muda mfupi bali janga la kijamii na kiuchumi kwa miezi na miaka ijayo.
Mladenov apongeza ushirikiano wa Israel na Palestian kukabili COVID-19
Mratibu maalum wa Umoja wa Mataifa katika mchakato wa amani ya Mashariki ya Kati Nikolay Mladenov amepongeza ushirika baina ya mamlaka ya Palestina na Israel katika kukabiliana na mlipuko wa virusi vya Corona, COVID-19.
Wafanyakazi wa afya ni askari wa mstari wa mbele dhidi ya COVID-19, tuwalinde
Askari wengi wameona vitisho vya vita kwa haraka, na ingawa ilikuwa ya kutisha mara nyingi, walijua ni nani wanapigana naye, na wangeweza kumtambua adui wao.
Andiko la Waziri wa afya wa Kenya Mutahi Kagwe na Siddharth Chatterjee, Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Kenya.
COVID-19 imeumbua nchi tajiri na maskini- ILO
Shirika la kazi duniani, ILO limesema kuwa janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19, limeweka hadharani udhaifu wa masoko ya ajira duniani.
UN yawajulisha nchi wanachama kuhusu mapambano dhidi ya COVID-19
Katika mkutano maalum kupitia njia ya mtandao uliofanyika leo Katibu Mkuu wa moja wa Mataifa, Rais wa Baraza Kuu la Umoja huo, Baraza la Usalama na baraza la kiuchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC wamezijulisha nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhusu juhudi za Umoja huo katika kupambana na virusi vipya vya Corona, COVID-19 na kuendelea na kazi muhimu ya shirika hilo duniani kote.
ITU na UNESCO washirikiana kuhakikisha elimu kwa wanafunzi
Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO limezindua muungano wa elimu wa kimataifa ili kuhakikisha wanafunzi walio nje ya shule kutokana na mlipuko wa virusi vya Corona, COVID-19 wanasoma kupitia teknolojia. John Kibego na taarifa zaidi
(TAARIFA YA JOHN KIBEGO)
Mlipuko wa COVID-19 unaathiri uwasilishaji wa mlo shuleni-WFP
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP leo limezindua ramani mpya ya kidijitali inayodhihirisha athari za virusi vya Corona, COVID-19 katika program zake za mlo mashuleni. Flora Nduicha na taarifa kamili
(TAARIFA YA FLORA NDUCHA)
Kwa mujibu wa WFP ramani hiyo ambayo ni ya “ufuatiliaji wa kimataifa wa mlo mashuleni wakati wa kufungwa shule kutokana na mlipuko wa COVID-19 inatoa inatoa maenedeleo mapya ya kila siku kuhusu kufungwa kwa shule na idadi ya Watoto ambao hawapati tena mlo mashuleni kutokana na janga hili la Corona.