Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19: Kufungwa kwa shule kunazua changamoto kwa wazazi na walezi kudhbiti watoto
Kutokana na kuenea kwa kasi kwa virusi vya corona, COVID-19 ambavyo vinashambulia mfumo wa upumuaji wa binadamu, serikali nyingiduniani zimelazimika kufunga shule ili kuwaepusha watoto na maambukizi ya ugonjwa huo hatari. Kufungwa kwa shule kunawafanya watoto kusalia katika makazi yao huku changamoto kwa wazazi au walezi ikiwa ni kuwadhibiti wasitoke kwenda kukutana na wenzao mtaani kushiriki michezo yao ya kawaida.
Fahamu ukweli kuhusu COVID-19
Tangu kuibuka kwa virusi vya corona, COVID-19, duniani kote watu wamekuwa nao wakiibua dhana mbalimbali potofu za kuhusu namna ya kujikinga au kutibu maambukizi ya virusi hivyo. Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO, kupitia wavuti wake pamoja na mengine, limechapisha baadhi ya dhana hizo potofu na kuzitolea ufafanuzi kama anavyosimulia Flora Nducha
(Taarifa ya Flora Nducha )
MONUSCO nayo mstari wa mbele katika kudhibiti COVID-19 DRC
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako idadi ya wagonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 ambao wamethibitishwa hadi leo hii ni 109 huku 8 (wanane) kati yao tayari wamefariki dunia, Umoja wa Mataifa umechukua hatua kuunga mkono hatua za serikali za kudhibiti kusambaa zaidi kwa virusi hivyo miongoni mwa wananchi wanaowahudumia na wafanyakazi wake.
Kenya yatangaza visa vipya vya COVID-19 na kufikisha idadi ya wagonjwa hadi 81
Wagojwa wawili ambao wamethibitishwa kupona virusi vya corona nchini Kenya wameonekaa hadharani kwa mara ya kwanza leo wakati wakizungumza kwa njia ya video na Rais Uhuru Kenyatta na kuonyeshwa kwenye runinga kadhaa nchini Kenya. Hata hivyo wizara ya afya nchini Kenya imatangaza uwepo kwa wagonjwa 22 zaidi wa virusi vya corana hii leo na kufanya idadi jumla kufikia wagonjwa 81. Jason Nyakundi anayo taarifa kamili
(TAARIFA YA JASON NYAKUNDI)
1 Aprili 2020
Assumpta Massoi : Hujambo na Karibu kusikiliza Jarida kutoka Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa, kutoka hapa New York Marekani.
JINGLE (04”)
ASSUMPTA:Ni Jumatano 01 Aprili mwaka 2020, mwenyeji wako studioni hii leo ni mimi ASSUMPTA MASSOI
1: Kenya yachukua hatua zaidi kudhibiti COVID-19, wakati wagonjwa wawili wakipona na wapya kuzuka
Chonde chonde tusiwasahau wakimbizi wa ndani wakati wa COVID-19:UN
Serikali zinapaswa kuongeza juhudi za hatua zake ili kuwalinda wakimbizi wa ndani milioni 40 kote duniani dhidi ya tishio la virusi vya Corona, COVIDI-19.
MONUSCO na harakati za kudhibiti kuenea kwa COVID-19 nchini DRC
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako idadi ya wagonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 ambao wamethibitishwa hadi leo hii ni 109 huku 8 (wanane) kati yao tayari wamefariki dunia, Umoja wa Mataifa umechukua hatua kuunga mkono hatua za serikali za kudhibiti kusambaa zaidi kwa virusi hivyo miongoni mwa wananchi wanaowahudumia na wafanyakazi wake.
Dhana potofu kuhusu kinga na tiba ya virusi vya corona, COVID-19
Tangu kuibuka kwa virusi vya corona, COVID-19, duniani kote watu wamekuwa nao wakiibua na dhana mbalimbali potofu za kuhusu namna ya kujikinga au kutibu maambukizi ya virusi hivyo. Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, kupitia wavuti wake pamoja na mengine, limechapisha dhana hizo potofu na kuzitolea ufafanuzi.
Kenya yachukua hatua zaidi kudhibiti COVID-19, wakati wagonjwa wawili wakipona na wapya kuzuka
Wagonjwa wawili ambao wamethibitishwa kupona virusi vya corona nchini Kenya wameonekana hadharani kwa mara ya kwanza leo wakati wakizungumza kwa njia ya video na Rais Uhuru Kenyatta na kuonyeshwa kwenye runinga kadhaa nchini Kenya. Hata hivyo wizara ya afya nchini Kenya imatangaza kuwepo kwa wagonjwa 22 zaidi wa virusi vya corana hii leo na kufanya idadi jumla kufikia wagonjwa 81.
Haki na afya ya wakimbizi, wahamiaji na wasio na utaifa inatakiwa kulindwa wakati wa kushughulikia COVID-19
Taarifa ya pamoja kwa vyombo vya habari iliyotolewa hii leo na Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR, pamoja na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la wahamiaji, IOM, la kuhudumia wakimbizi UNHCR na la afya WHO imetoa wito kwa dunia kulinda haki na afya ya wakimbizi, wahamiaji na wasio na utaifa katika wakati huu wa mapambano dhidi ya virusi vya corona, COVID-19.