Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19 isiwe chanzo cha kusahau huduma muhimu za chanjo kwa watoto- UNICEF
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesihi serikali duniani kote kuanza mipango thabiti ya utoaji chanjo kwa watoto pindi janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 litakapodhibitiwa.
COVID-19: Zanzibar yachukua hatua kupunguza mlundikano magerezani
Idadi ya wagonjwa wa virusi vya Corona, huko visiwani Zanzibar nchini Tanzania ikiwa imefikia wagonjwa wawili, hii leo serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetangaza hatua za kuhakikisha sekta ya mahakama inaunga mkono hatua za kudhibiti kuenea kwa virusi vya Corona, COVID-19 ikiwemo kusitisha kwa muda usikilizaji wa kesi za madai na jinai. Omar Abdalla wa Televisheni washirika ZenjFM kutoka Zanzibar ametuandalia taarifa hii.
Jinsi ya kuzungumza na watoto kuhusu ugonjwa wa virusi vya Corona
Ni rahisi sana kuhisi kuzidiwa uwezo na kila kitu pindi unaposikia kuhusu ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19. Ni wazi kuwa watoto wanapata shaka na shuku hasa wanapoona taarifa kwenye runinga au kusikia kutoka kwa watu. Je utazungumza nao vipi? Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limekupatia vidokezo vifuatavyo ili uweze kuibua mjadala na watoto na kuzungumza nao.
COVID-19: Mradi wa UN-Habitat wafanikisha unawaji mikono Mathare, Kenya
Shirika la makazi la Umoja wa Mataifa, UN-Habitat kwa kushirikiana na kituo cha mazingira cha vijana eneo la Mathare jijini Nairobi, Kenya, au Mathare Environmental One Stop Youth Centre wameungana kwa ajili ya kutoa huduma ya maji safi ya kunawa mikono kwa wakazi 50,000 wa kijiji cha Mlango Kubwa katika mtaa wa Mathare ulioko kwenye mji mkuu wa Kenya, Nairobi. Taarifa kamili na Grace Kaneiya.
(Taarifa ya Grace)
Video ya UN-Habitat inaonesha wakazi wa Kijiji cha Mlango Kubwa kwenye mtaa wa Mathare katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, wakiendelea na shughuli za kila siku.
UN yazindua ombi la dola bilioni 2 kusadia nchi maskini kukabili virusi vya Corona
Umoja wa Mataifa leo umezindua ombi la dola bilioni 2 ili kusaidia harakati za kukabiliana na ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 katika nchi maskini zaidi duniani.
Mradi wa pamoja wa UN-Habitat ni msaada kwa wakazi wa mtaa wa Mathare, Kenya
Nchini Kenya hatua zaidi zimechukuliwa kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19, wakati wakati huu ambapo tayari serikali imethibitisha kuwepo kwa wagonjwa 28 wa ugonjwa huo.
COVID-19: Uganda yapiga marufuku wakimbizi kuingia nchini humo
Serikali ya Uganda imesema kutokana na kuenea kwa ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19, na idadi ya wagonjwa kufikia 14, wakimbizi hivi sasa hawataingia nchini humo huku ikizuia hata huduma za kudhibiti kuenea kwa virusi hivyo zilizokuwa zikitolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kwenye vituo vya mapokezi ya wakimbizi.
Magereza na rumande zipunguze mirundikano kuepusha kusambaa COVID-19
Ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 umeanza kusambaa kwenye magereza, vituo vya ushikiliaji wahamiaji wasio na nyaraka na hivyo serikali lazima zichukue hatua kulinda afya za wanaoshikiliwa kwenye maeneo hayo, amesema Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu kwenye Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet.
Yemen sitisheni uhasama mjikite na COVID-19:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito kwa pande kinzani katika mzozo wa Yemen kusitisha uhasama mara moja na kujikita katika majadiliano ya suluhu ya kisiasa huku wakifanya kila wawezalo kukabiliana na virusi vya Corona, COVID-19.