Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Mtazamo wa maeneo ya forodhani visiwani Zanzibar.
UN News/Assumpta Massoi

COVID-19: Zanzibar yachukua hatua kupunguza mlundikano magerezani

Idadi ya wagonjwa wa virusi vya Corona, huko visiwani Zanzibar nchini Tanzania ikiwa imefikia wagonjwa wawili, hii leo serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetangaza hatua za kuhakikisha sekta ya mahakama inaunga mkono hatua za kudhibiti kuenea kwa virusi vya Corona, COVID-19 ikiwemo kusitisha kwa muda usikilizaji wa kesi za madai na jinai. Omar Abdalla wa Televisheni washirika ZenjFM  kutoka Zanzibar ametuandalia taarifa hii.

Sauti
2'47"
Watoto wa shule sehemu za Beni -DRC wajifunza kuwa kuosha mikono ndiyo njia bora ya kujilinda dhidi ya magonjwa ikiwemo Ebola
UNICEF/Thomas Nybo

Jinsi ya kuzungumza na watoto kuhusu ugonjwa wa virusi vya Corona

Ni rahisi sana kuhisi kuzidiwa uwezo na kila kitu pindi unaposikia kuhusu ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19. Ni wazi kuwa watoto wanapata shaka na shuku hasa wanapoona taarifa kwenye runinga au kusikia kutoka kwa watu. Je utazungumza nao vipi? Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limekupatia vidokezo vifuatavyo ili uweze kuibua mjadala na watoto na kuzungumza nao.

© Julius Mwelu/ UN-Habitat

COVID-19: Mradi wa UN-Habitat wafanikisha unawaji mikono Mathare, Kenya

Shirika la makazi la Umoja wa Mataifa, UN-Habitat kwa kushirikiana na kituo cha mazingira cha vijana eneo la Mathare jijini Nairobi, Kenya, au  Mathare Environmental One Stop Youth Centre wameungana kwa ajili ya kutoa huduma ya maji safi ya kunawa mikono kwa wakazi 50,000 wa kijiji cha Mlango Kubwa katika mtaa wa Mathare ulioko kwenye mji mkuu wa Kenya, Nairobi. Taarifa kamili na Grace Kaneiya.
(Taarifa ya Grace)
Video ya UN-Habitat inaonesha wakazi wa Kijiji cha Mlango Kubwa kwenye mtaa wa Mathare katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, wakiendelea na shughuli za kila siku. 

Audio Duration
1'26"