Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Mwanamke akiwa amembeba binti yake katika kituo cha Wisdom kilichopo eneo la Gurei mjini Juba nchini Sudan kusini baada ya kupigwa na mumewe.
© UNICEF/Albert Gonzalez Farran

Ukatili majumbani ukiongezeka, Katibu Mkuu wa UN ataka sitisho la vitendo hivyo

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito wa hatua za kukomesha ghasia na ukatili majumbani dhidi ya wanawake na wasichana, kufuatia ripoti kuwa vitendo hivyo vimeshamiri hivi sasa maeneo mbali mbali duniani baada ya serikali kutaka wananchi wasalie majumbani kuepusha kuenea kwa ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19.

Sauti
2'9"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akizungumza na waanishi wahabari kupitia mtandao
UN Photo/Loey Felipe

Ni wakati wa kugeuza maneno kuwa vitendo kusitisha uhasama:UN

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema wito wake wa kimataifa alioutoa wiki iliyopita wa kusitisha uhasama umepokelewa vyema kote duniani lakini ameonya kwamba kuna pengo kubwa kati ya azma na uteekelezaji na kusisitiza kwamba ili kunyamazisha silaha ni lazima kupaza sauti kwa ajili ya amani na kugeuza maneno kuwa vitendo.

Mradi wa sehemu ya kunawa mikono kwa ufadhili wa Mo Dewj Foundation nchini Tanzania.
UN News/ UNIC Dar es Salaam

Hospitali ya taifa Tanzania, Muhimbili yatenga sehemu maalum kwa ajili ya kunawa mikono

Tanzania kama ilivyo katika mataifa mengine imeweka mikakati kwa ajili ya kudhibiti kuenea kwa virusi vya corona au COVID-19. Hatua mbali mbali zinachukuliwa na serikali na pia mashirika binafsi yanaunga mkono juhudi za serikali. Afisa wa maswasiliano wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa jijini Dar es Saalam, UNIC ametembelea hospital ya taifa ya Muhimbili kushuhudia baadhi ya mikakati iliyowekwa kama sehemu ya juhudi za kudhibiti kuenea kwa virusi hivyo

Sauti
2'51"