Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

Warren Bright/UNFPA Tanzania

Vijana wasichana na wavulana mkoani Mara wasimama kidete kukabiliana na FGM

Umoja wa Mataifa kupitia lengo namba 5 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs la usawa wa kijinsia, ukipaza sauti hatua zichukuliwe ili kutokomeza kitendo cha ukeketaji wa watoto wa kike na wanawake, mkoani Mara nchini Tanzania tayari hatua zinachukuliwa na zinazaa matunda. Mafunzo kwenye kituo cha ushirika wa kutokomeza ukeketaji, ATFGM kilichopo  kijiji cha Masanga yamekuwa ni chachu ya kutekeleza wito huo kwa kuwa wasichana kwa wavulana wanapata mafunzo ya kuwawezesha kuepukana na tohara na ukeketaji ambao unahatarisha maisha yao.

Sauti
4'10"
UNIC/Stella Vuzo

Mwalimu wa kike aanzisha biashara inayotoa fursa za ajira kwa wengine Uganda

Wanawake wanajumuisha takriban asilimia 52.5 ya nguvu kazi na ni kiungo muhimu katika kufanikisha melengo ya maendeleo endelevu, SDGs, hususan katika sekta ya ujasiriamali kwenye biashara ndogo ndogo na za wastani. Hata hivyo, wanawake kwa kawaida hukabiliwa na changamoto nyingi ikilinganishwa na wanaume katika kuanzisha, kusimamia na kukuza biashahra hizo kwa mujibu wa ripoti ya shirika la kazi ulimwenguni, ILO, iliyoangazia uwekezaji wa wanawake na mapendekezo nchini Uganda mwaka 2014.

Sauti
3'59"
Photo: UN/DPI Photo

Watu wa asili ni wahifadhi wa maeneo yao ya asili na si wavurugaji- Dkt. Ogada

Vuta  nikuvute kati ya watu wa jamii ya asili na wanyama imekuwa ikiendelea maeneo mbalimbali duniani ambako serikali zinataka kuhifadhi wanyama huku watu wa asili nao wakisema uasili wao unaendana na mazingira waliyomo, hivyo wanapaswa kusalia kwenye mazingira hayo. Ni kwa kuzingatia mvutano huo hivi karibuni wakati wa mkutano wa jopo la wataalamu wa masuala ya watu wa jamii za asili huko Nairobi, Kenya, Newton Kanhema wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa nchini humo, UNIC Nairobi, alimsaka Dkt.

Sauti
4'24"
UN/maktaba

Ndoto yangu imetimia, nitajitahidi kwa kadri ya uwezo wangu- Mtoto Rehema

Hatimaye mtoto Rehema Paul ambaye aliponea chupuchupu kuajiriwa kazi za ndani baada ya mwajiri wake kubaini kuwa umri wake  haukuwa unaruhusu kufanya kazi, sasa ameanza masomo katika shule ya msingi Mchikichini, kwenye manispaa ya Morogoro nchini Tanzania. Mwajiri huyo, Herieth Mkaanga amefurahi sana kwani amefanikisha lengo namba 4 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs la kutaka elimu kwa watoto bila ubaguzi wowote ule na wakati huo huo kufanikisha ndoto ya mtoto Rehema ya kupata elimu.

Audio Duration
4'24"
UN

Natumia uelewa wangu kuhusu mauaji ya halaiki kuepusha yasiyotokee tena- Mwanafunzi Tanzania

Miaka 74 tangu kukombolewa kwa kambi ya mateso na mauaji ya wayahudi milioni Sita huko  Auschwitz-Birkenau, nchini Poland yaliyofanywa na manazi wa Ujerumani, bado kuna ubaguzi kwa misingi mbalimbali iwe ya kidini au kikabila. Hali hii  hutia sana wasiwasi Umoja wa Mataifa ambao uliamua siyo tu kutenga siku ya kimataifa ya kumbukizi ya mauaji hayo ya halaiki dhidi ya wayahudi kama fursa ya kukumbuka na kutathmini, bali pia kuwa na programu maalum ya kuelimisha jamii juu ya madhila ya mauaji ya aina hiyo na viashiria vyake ili kuepusha yasitokee tena.

Sauti
4'5"
UNEP GRID Arendal/Peter Prokosch

Maarifa ya jamii za asili huziwezesha kuishi vyema na wanyamapori

Watu wa jamii za asili mara kwa mara wameelezea wasiwasi wao kuhusu juhudi za kuhifadhi mazingira kutozingatia haki na maarifa ya kundi hilo. Jamii hiyo hutolea mifano harakati za kutengwaa maeneo ya uhifadhi ambapo inasema kuwa husababisha watu hao kufurushwa makwao na hata kupoteza kipato. Changamoto hiyo iliangaziwa kwenye ripoti ya mwaka 2016 ya mtaalam huru wa haki za watu wa asili na ilijadiliwa mwaka 2018 katika kikao cha kudumu cha watu wa asili.

Sauti
4'7"
World Bank/Charlotte Kesl

Ubunifu wa ajira wazaa matunda kwa vijana nchini Burundi

Kubuni ajira ni swala linalotatiza pakubwa vijana wengi barani Afrika. Wengi hulalamikia ukosefu wa mitaji au chanzo cha kuanzisha biashara. Lakini wataalamu wa biashara na wachanganuzi wa miradi  wanaamini kuwa mtaji mkubwa na wa kuaminika kwanza ni  fikra ya biashara  pamoja na kujumuika katika shirika.

Kundi moja la vijana wapatao 50 nchini Burundi  kwa jina la CVC, baada ya kupokea  mafunzo ya mtaalamu wameanza kuona mafaanikio  ya biashara yao ilioanza  tu na unga wa uji.

Sauti
3'52"