Walinda amani wanaondoka Mali lakini Umoja wa Mataifa unabakia
Pakua
Baada ya kuweko nchini Mali kwa muongo mmoja, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani na kuweka utulivu nchini humo umeanza kufunga virago. Hii ni baada ya mamlaka nchini humo kutaka ujumbe huo uondoke, ombi ambalo liliridhiwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Sasa MINUSMA inatakiwa iwe imeondoka ifikapo tarehe 31 mwezi Agosti mwaka huu. Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Mali, El-Ghassim Wane ambaye pia ni Mkuu wa MINUSMA amezungumza na Jerome Bernard wa Idhaa ya Kifaransa ya Umoja wa Mataifa, mazungmzo ambayo ndio msingi wa makala hii inayoletwa kwako na Assumpta Massoi.
Audio Credit
Leah Mushi/Assumpta Massoi
Audio Duration
3'40"