Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MONUSCO na ufanikishaji wa uchaguzi mkuu wa 2023 DRC

MONUSCO na ufanikishaji wa uchaguzi mkuu wa 2023 DRC

Pakua

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, (MONUSCO) unashiriki katika maandalizi ya uchaguzi mkuu nchini humo unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu ambapo tayari umeshasaidia usafirishaji wa nyaraka za uchaguzi, halikadhalika mafunzo kwa polisi wa kitaifa ili uchaguzi huo uwe huru na ufanyike kwa amani.

Ikumbukwe kuwa wiki iliyopita, Rais wa DRC Félix Antoine Tshisekedi Tshilombo akihutubia mjadala mkuu wa mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani alithibitisha kuwa uchaguzi mkuu wa rais, wabunge, magavana na madiwani utafanyika kama ilivyopangwa na Tume Huru ya Uchaguzi nchini humo, CENI tayari imeshaanza kuchapisha majina ya wagombea.

Tumesafirisha nyaraka nyeti za CENI

Akizungumza George Musubao wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa mjini Beni, jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC, Msemaji wa MONUSCO mjini Beni-Lubero Bwana Jean Tobie Okala amesema “CENI  inatuambia inabidi zifanyike kwa hali ya usalama na amani. Jambo la kwanza ni kuungwa mkono kwa CENI. Nakujulisha kwamba tangu Januari 2023 MONUSCO imesafirisha maelfu ya tani za shehena nyeti sana za uchaguzi ambazo ni za CENI na ambazo zimewezesha shughuli za kurekodi na kuandikisha wapiga.”

Audio Credit
George Musubao
Audio Duration
4'53"
Photo Credit
UN News/George Musubao