Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mradi wa "Football for the Goals" kufanikisha malengo 17 ya maendeleo endelevu Rwanda - UN Rwanda

Mradi wa "Football for the Goals" kufanikisha malengo 17 ya maendeleo endelevu Rwanda - UN Rwanda

Pakua

Umoja wa Mataifa umekuwa ukipigia chepuo mbinu mbali mbali halali za kufanikisha malengo 17 ya maendeleo endelevu, SDGs, na miongoni mwa mbinu hizo ni mpira wa miguu, soka, wengine wakisema kabumbu au kandanda! Sasa wenyewe wabobezi au manguli wa soka wameitikia wito na Umoja wa Mataifa hususan nchini Rwanda ukaitikia Naam!!! Je nini kinafanyika? Assumpta Massoi wa Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa ameketi na Mkuu wa Ofisi ya Mratibu Mkazi wa UN, Rwanda Josephine Marealle-Ulimwengu na anafafanua kitendawili hicho.

Audio Credit
Anold Kayanda/Assumpta Massoi
Audio Duration
6'43"
Photo Credit
UN News