Ujumuishwaji ni msingi mkuu katika kusongesha malengo ya maendeleo endevu - Waheshimiwa Baraza na Mugabe
Pakua
Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa kuhusu malengo ya maendeleo endelevu lijulikanalo kama HLPF linafikia tamati hii leo hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York-Marekani. Wawakilishi wa nchi na serikali, wanasayansi, wanazuoni, mashirika ya umoja wa Mataifa, asasi mbalimbali na vijana wamekutana kuanzia tarehe 10 Julai kujadili hatua za kuchukua ili kuhakikisha malengo hayo muhimu ya maendeleo yanatimizwa ifikapo mwaka 2030. Leah Mushi ameketi chini na Gavana wa Kauti ya Kakamega Fernandes Baraza pamoja na Mbunge wa Likuyani Innocent Mugabe wote kutoka nchini Kenya kuzungumza nini wanaondoka nacho baada ya Siku 10 za mkutano huu.
Audio Credit
Flora Nducha/Leah Mushi
Audio Duration
8'15"