Fistula bado tatizo, UNFPA Tanzania wapania kuitokomeza
Fistula! Ugonjwa unaowakumba wanawake na wasichana kutokana na kuchelewa kupata huduma stahiki wakati wa kujifungua. Takwimu zinaonyesha kuwa licha ya mafanikio katika mbinu za kisasa za kutoa huduma ya afya bado takriban wanawake 800 wanafariki dunia kutokana na maradhi yatokanayo na uja uzito kila siku na kwa kila mwanamke anayefariki takriban wanawake 20 wanapata majeraha ya maisha kama vile fistula.