Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano

Homa ya ini bado ni changamoto Uganda

Tarehe ishirini na nane Julai kila mwaka dunia huadhimisha siku ya homa ya ini. Shirika la afya ulimwenguni WHO huitumia siku hiyo kuhamasisha makabiliano dhidi ya ugonjwa huo hatari.

Katika maadhimisho ya mwaka huu, WHO inazitaka nchi wanachama kuchukua hatua haraka kuboresha ufahamu kuhusu homa ya ini, kuongeza fursa ya kufanyiwa vipimo na kupata huduma ya tiba.

Duniani kote watu milioni 40 wameambukizwa homa ya ini aina B na C, ikiwa ni mara 10 zaidi ya watu wanaoishi na VVU.

Tumenuia kutokomeza homa ya ini ifikapo 2030: Tanzania

Tarehe 28 mwezi Julai kila mwaka dunia inaadhimisha Siku ya Ugojwa wa Homa ya Ini. Ugonjwa huu unaongoza kwa maambukizi ukilinganishwa na virusi vya Ukimwi, lakini wengi hawautambui hata kuchukua hatua dhidi yake. Hii ni kauli ya shirika la afya ulimweguni WHO linalozihamasisha nchi wanachama kuchua hatua za tiba na elimu hima.

Kwa mujibu wa WHO watu milioni 40 Duniani kote wameambukizwa homa ya ini aina B na C, ikiwa ni mara 10 zaidi ya watu wanaoishi na VVU.

Tumeoanisha maono ya 2030 ya Kenya na SDGs- waziri Kiunjuri

Wakati ripoti ya kwanza kabisa kuhusu malengo ya maendeleo endelevu imezinduliwa jijini New York, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon amesema ripoti hiyo ni taswira ya hali halisi ya hatua zilizopigwa duniani katika utekelezaji wa  ajenda ya mwaka 2030 malengo ya maendeleo endelevu.

Katibu Mkuu amesema takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kwamba mtu mmoja kati ya watu wanane anaishi katika umaskini uliokithiri, huku takriban milioni mia nane wakikabiliwa na njaa.

Wasichana vigori wanamchango mkubwa katika jamii:Musoti-UNFPA

[caption id="attachment_289755" align="alignleft" width="300"]mahojianounfpa

Juma hili shirika la Umoja wa mataifa la idadi ya watu duniani UNFPA limeadhimisha siku ya idadi ya watu duniani , kwa kauli mbiu ya kutoa msukomu wa kuwawezesha wasichana vigori.  Kwa mujibu wa shirika hilo kundi hilo lwa vijana linakabiliwa na changamoto nyingi , na itakuwa vigumu kutimiza ajenda ya mwaka 2030 ya maendeleo endelevu kama litaachwa nyuma.

#UNCTAD14 vijana wajumuishwa, wanawake kuangaziwa- Dkt. Kituyi

Baada ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kupitisha makubaliano kadhaa muhimu mwaka jana ikiwemo ajenda ya maendeleo endelevu na mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, kauli muhimu hivi sasa ni kwamba hakuna anayepaswa kuachwa nyuma. Kila mkazi wa sayari ya dunia awe mwanamke, mwanaume, mtoto au mzee anapaswa kujumuika na kujumuishwa kwenye mipango ya maendeleo kwa ustawi wa wote.

Wanyama watishia uvuvi na ufugaji, Uganda

Licha ya ukweli kwamba wanyama ni rafiki wa binadamu  na hutumiwa kama sehemu ya kitoweo, baadhi yao hususani wanayama pori wamekuwa  kikwazo kwa binadamu kujipatia riziki.

Nchini Uganda tunaelezwa kuwa shughuli za uvuvi na ufugaji zinakwamishwa na wanayama pori. Kulikoni? Ungana an John Kibego.

Madhila ya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu nchini Burundi

Usaidizi kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu ni moja ya jukumu la Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la kuhudumia watoto UNICEF na wadau wengine ikiwemo nchi wanachama na asasi za kiraia.

Barani Afrika husuani Afrika Mashariki Watoto hawa hufahamika zaidi kama watoto wa mitaani ikibeba tafsiri ya watoto wasio na mwenyewe yaani wazazi, walezi au jamii na mamlaka za nchi zimewatelekeza na hivyo kuishia kuishi mitaani.

Makubaliano ya amani yaleta matumaini kwa muziki wa kiasili wa Vallenato Colombia

Mnamo mwaka 1982, Gabriel Garcia Marquez, mwandishi mashuhuri kutoka Colombia alipokea tuzo ya Nobel katika Fasihi. Manthari iliyotamalaki wakati akipokea tuzo hiyo mjini Oslo, Norway, ilikuwa ya ngoma ya kitamaduni kutoka pwani ya kaskazini mwa Colombia, iitwayo Vallenato. Je, Vallenato ndiyo ipi? Kufahamu zaidi, ungana na Joshua Mmali akikupeleka hadi Colombia, katika makala hii

Hofu yatanda kila uchao kwa wapalestina ukingo wa magharibi wa mto Jordan

Huko ukingo wa magharibi wa mto Jordan, baadhi ya wapalestina wanaishi kwa hofu kubwa kila uchao. Hii ni kutokana na mashambulizi ya kulipiza kisasi yanayofanywa na Israel kutokana na kile inachoeleza kuwa ni mashambulizi yanayofanywa na wapalestina dhidi ya waisraeli. Hali ni zaidi ya kuviziana lakini kama wasemavyo wahenga, vita vya panzi, yaumiayo ni majani. Je ni nani hasa wanaoathiriwa na hali hiyo? Assumpta Massoi anakupeleka huko Mashariki ya Kati kupitia makala hii.