Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano

Ugonjwa wa malaria na juhudi za kuutokomeza Tanzania

Tarehe 25 mwezi Aprili ya kila mwaka, dunia huadhimisha siku ya malaria, msisistizo ukiwa kutokomeza ugonjwa huo. Kwa mujibu wa takwimu za shirika la afya ulimwenguniWHO, takribani watu bilioni 3.2 ambayo ni karibu nusu ya idadi ya watu duniani wako katika hatari ya kuambikizwa malaria.

Mwaka 2015 visa zaidi ya milioni 200 vya malaria viliripotiwa na zaidi ya vifo Laki Nne. Bara la Afrika hususani nchi za kusini mwa jangwa la Sahara zinabeba mzigo mkubwa ambapo WHO inasema kwamba mwaka 2015 bara hilo lilikuwa na asilimia 89 ya visa vya malaria na asilimia 91 ya vifo.

Mabadiliko ya tabianchi barani Asia, hatua zachukuliwa.

Takribani wiki moja baada ya kusainiwa kwa mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi mjini New York, Marekani  madhara ya suala hilo barani Asia ni dhahiri lakini jumuiya ya kimataifa inahaha kunusuru wakulima na uhakika wa chakula barani humo. Ungana na Joseph Msami katika makala itakayokupeleka kueneo hilo ili kupata taswira ya madhara na hatua zinazochukuliwa nchini Cambodia.

Lazima kujumuisha makundi yote katika ujenzi wa amani: Kamau

Harakati za ujenzi wa amani ni vyema zijumuishe makundi yote ikiwemo makabila madogo,  amesema mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Mataifa ya ujenzi wa amani PCB ambaye pia ni mwakilishi wa kudumu wa Kenya katika ofisi za Umoja wa Mataifa mjini New York, Balozi Macharia Kamau. Katika mahojiano maaluma na Joseph Msami kuhusu maazimio ya aina yake ya ujenzi wa amani baada ya mizozo, yaliyopitishwa leo na baraza la usalama na baraza kuu, Balozi Kamau anaanza kueleza umuhimu wake.

Msichana aliyekombolewa kutoka Boko Haram aeleza machungu

Nchini Nigeria takribani wanawake na wasichana 2000 wametekwa nyara na kikundi cha kigaidi cha Boko Haram tangu mwaka 2012.Miongoni mwao ni Khadija ambaye akiwa na umri wa miaka 17 alitekwa nyara na kulazimishwa kuolewa na magaidi hao wa Boko Haram. Je ni madhila yapi alipitia akiwa huko utumwani? Na hadi sasa nini kinamtia machungu kila uchao? Assumpta Massoi anakusimulia katika makala hii iliyowezeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF.

Hatuna uchaguzi katika kudhibiti mabadiliko ya tabianchi- Balozi Manongi

Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo kwazo athari za mabadiliko ya tabianchi ziko dhahiri. Mathalani kuongezeka kwa kiwango cha maji ya bahari na hivyo kutishia uwepo wa visiwa, halikadhalika mizozo kati ya wakulima na wafugaji katika kusaka malisho. Je nini kinafanyika na je kutiwa saini mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi kunaashiria nini? Balozi Tuvako Manongi, mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa amezungumza na Assumpta Massoi wa Idhaa hii kabla ya kutia saini mkataba huo kwa niaba ya nchi yake. Hapa anaanza kwa kuelezea athari za mazingira Tanzania.

Picha:MJUMITA

Twatiwa moyo na utiwaji saini mkataba wa tabianchi- MJUMITA

Tarehe 22 Aprili mwaka 2016 ni siku ya kihistoria kwa Umoja wa Mataifa na nchi wanachama bila kusahau watetezi wa uhifadhi wa mazingira kwa kuwa mkataba wa tabianchi  utatiwa saini kwenye makao makuu ya Umoja huo New  York, Marekani. Utiaji saini huo unafanyika huku wadau wa mazingira kama vile mtandao wa usimamizi wa misitu Tanzania, MJUMITA ukiwa nao mstari wa mbele kulinda mazingira hususan maeneo ya misitu yaliyo karibu na wananchi.

Askari MONUSCO wasaidia raia DRC

Askari wa kulinda amani wa ujumbe wa  Umoja wa Mataifa  nchini Jamhuri ya Kidemkorasia ya Congo DRC MONUSCO kimetoa misaada kadhaa kwa jamii nchini humo.

Misaada hiyo katika sekta ya elimu na kwa wakimbizi imepokelewa kwa bashasha na wakazi nchini humo kama anavyosimulia Joseph Msami. Ungana naye.

UNESCO yasaidia kutoa mafunzo kwa wanahabari Yemen

Nchini Yemen, sekta ya uandishi wa habari inakabiliwa na changamoto nyingi, hususan wakati huu ambapo mgogoro wa kisiasa bado unatokota nchini humo. Waandishi nchini humo wanafanya kazi katika mazingira magumu, changamoto kubwa zaidi ikiwa ni usalama wao.

Kutokana na mazingira hayo, Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, liliandaa hivi karibuni warsha ya mafunzo kwa wanahabari wa Yemen, chini ya mamlaka yake ya kuendeleza uhuru wa kujieleza na upatikanaji taarifa.

UN Photo/Paulo Filgueiras

Mchango wa biashara ya utumwa katika muziki wa Amerika ya Kusini

Kila mwaka Machi 25, Umoja wa Mataifa huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kumbukumbu ya Waathirika wa Utumwa na biashara ya utumwa.

Katika Umoja wa Mataifa, siku hii imeleta fursa ya kuelimisha jamii juu ya sababu zake, madhara yake na kuongeza ufahamu wa hatari ya ubaguzi wa rangi na ubaguzi mamboleo na jinsi ya kupambana nayo. Mwaka huu, moja ya hafla za kumbukumbu iliangazia jinsi biashara ya utumwa ilivyochangia katika muziki wa watu wenye asili ya kiafrika hususan Amerika ya Kusini. Assumpta Massoi anakufahamisha zaidi katika makala hii...

Kwa nini hedhi iwe kikwazo kwa mtoto wa kike kusoma?

Lengo namba Nne la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linatoa wito kwa kila mkazi wa dunia bila kujali jinsia au hali ya kiafya ikiwemo mzunguko wa hedhi kwa wasichana.

Kama hiyo haitoshi lengo namba Tano linataka usawa wa kijinsia na kujenga uwezo kwa wasichana na wanawake hviyo basi elimu kwa wasichana barubaru ni msingi wa kufanikisha malengo haya. Je harakati zipi zinafanyika?