Ajali ya barabarani hukwamisha uwezo wa manusura wa ajali
Ripoti ya hali ya usalama barabarani ya mwaka 2015 ikiangazia mataifa 180 inasema kwamba idadi ya vifo vitokanavyo na ajali za barabarani imeongezela huku maafa mengi yakishuhudiwa nchi za kipato cha chini.
Kutokana na hali hiyo, katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita mataifa yalipanga sheria angalau moja kuambatana na sheria za barabarani ikiwemo: kufunga mkanda, dereva kutotumia mihadarati na kuzingatia mwendo kasi.