29 Mei 2020
Kwenye Jarida la Umoja wa Mataifa leo ni siku ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa duniani :
-kwenye mada yetu ya kina baadhi ya wanawake wakazi wa mji wa Beni, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wameomba walinda amani wanawake kutoka Tanzania waendelee kuwaunga mkono kiuchumi na kijamii.
-Mlinda amani mwanamke kutoka Tanzania ambaye anahudumu katika ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, MONUSCO amethibitisha umuhimu wa uwepo wa askari wa kike katika ulinzi wa amani