Mtalaam wa UM apata hasira kuhusu mauaji ya mpalestina Hebron
Video ya raia wa Palestina aliyeuawa na askari wa Israel akiwa amejeruhiwa na kulala chini imemtia hasira mratibu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu mauaji ya kiholela Christof Heyns.
Hii ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo kufuatia mauaji yaliyofanyika wili iliyopita mjini Hebron, kwenye ukingo wa magharibi, yakiripotiwa na shirika la haki za binadamu la Israel ambalo lilitoa video hiyo. Ripoti inaeleza kwamba mpalestina huyo amepigwa risasi baada ya kumchoma kisu askari wa Israel.