Baraza la Usalama lapitisha azimio la kudhibiti uuzaji wa mafuta na silaha Libya
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, leo limepitisha azimio la kuongeza muda wa mamlaka ya vikwazo vilivyowekewa Libya chini ya azimio lake namba 2146 la mwaka 2014, hadi Julai 31 mwaka 2017.
Baraza la Usalama pia limelaani majaribio ya uuzaji haramu wa mafuta ghafi ya Libya nje, ukiwemo ule unaofanywa na taasisi ambazo hazipo chini ya mamlaka ya serikali ya makubaliano ya kitaifa (GNA).