Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UN Photo/Iason Foounten

Baraza la Usalama lapitisha azimio la kudhibiti uuzaji wa mafuta na silaha Libya

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, leo limepitisha azimio la kuongeza muda wa mamlaka ya vikwazo vilivyowekewa Libya chini ya azimio lake namba 2146 la mwaka 2014, hadi Julai 31 mwaka 2017.

Baraza la Usalama pia limelaani majaribio ya uuzaji haramu wa mafuta ghafi ya Libya nje, ukiwemo ule unaofanywa na taasisi ambazo hazipo chini ya mamlaka ya serikali ya makubaliano ya kitaifa (GNA).

Watu wanaohitaji misaada maeneo yaliyozingirwa Syria bado hawaipati:UM

Nchini Syria maelfu tya watu ambao wanahitaji misaada ya haraka bado haiwafikii katika baadhi ya maeneo yaliyozingirwa umesema Umoja wa mataifa Alhamisi. Amina Hassan na taarifa kamili.

(TAARIFA YA AMINA)

Kwa mujibu wa Jan Egeland, ambaye ni mratibu wa misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Syria , kuna hali ya taharuki kwamba kazi ya awali ambayo ilisaidia misafara ya misaada kuwafikia watu wanaoihitaji  nchini Syria sasa imepungua.

Mkuu wa MINUSCA akariri msimamo wake dhidi ya ukatili wa kingono

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, Parfait Onanga-Anyanga, amelezea dhiki yake kuhusu vitendo vya ukatili wa kingono vilivyoripotiwa kufanyika na walinda amani wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa anaoongoza nchini humo, MINUSCA.

Kwenye makala aliyoandika katika gazeti la Newsweek, Bwana Onanga-Anyanga ameeleza kwamba siku chache zilizopita alipokea taarifa ya kesi nyingine ya ubakaji dhidi ya msichana mwenye umri wa miaka 14, ambayo inafuatia ripoti za vitendo vingine kadhaa vilivyoripotiwa kufanyika mwaka 2014 na 2015.

Usalama ndio ufunguo wa maendeleo ya nishati ya nyuklia- IAEA

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA), Yukiya Amano, amesema leo kuwa usalama ni suala muhimu kwa maendeleo ya nishati ya nyuklia katika siku zijazo.

Amano amesema hayo akihutubia mkutano wa 2016 kuhusu sekta ya nyuklia, ambao unamulika udhibiti wa vitisho vya kupitia kwenye mtandao wa intaneti, kudumisha usalama wa matumizi, hifadhi na usafirishaji wa bidhaa za minururisho na za nyuklia, pamoja na mchango wa sekta ya nyuklia duniani.

Mtalaam wa UM apata hasira kuhusu mauaji ya mpalestina Hebron

Video ya raia wa Palestina aliyeuawa na askari wa Israel akiwa amejeruhiwa na kulala chini imemtia hasira mratibu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu mauaji ya kiholela Christof Heyns.

Hii ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo kufuatia mauaji yaliyofanyika wili iliyopita mjini Hebron, kwenye ukingo wa magharibi, yakiripotiwa na shirika la haki za binadamu la Israel ambalo lilitoa video hiyo. Ripoti inaeleza kwamba mpalestina huyo amepigwa risasi baada ya kumchoma kisu askari wa Israel.

Ulinzi wa mambo ya kale ni suala la kimataifa:UNESCO

Ulinzi wa kazi za kihistoria za Sanaa sio tu suala la wakati wa migogoro au vita bali ni suala linalotia hofu kimataifa limesema shirika la Umoja wa mataifa la Elimu , Sayansi na Utamaduni UNESCO.

Huo pia ni mtazamo wa Dr Donna Yates mhadhiri wa usafirishaji haramu wa mambo ya kale na uhalifu wa Sanaa katika chuo kikuu cha Glasgow nchini Scotland.

Dr Yates anashiriki majadiliano kuhusu usafirishaji wa mali za kitamaduni yaliyoandaliwa na UNESCO mjini Paris leo Jumatano. Anaelezea ni maeneo gani hasa yaliyo katika hatari ya kuporwa.

(SAUTI YA DR YATES 1)

MONUSCO yaongezwa mwaka mmoja DRC

Baraza la Usalama leo limepitisha azimio la kuongeza muda wa mamlaka ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC MONUSCO kwa mwaka mmoja hadi Machi, 31, 2017, pia likiamua kutopunguza zaidi idadi ya walinda amani, hadi hali ya usalama itakapoimarika.

UN Photo/Iason Foounten

Kobler alaani mauaji ya raia Libya

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Libya, Martin Kobler, amelaani mauaji yaliyoripotiwa kufanyika Mashariki mwa Libya kwenye maeneo ya al-Tewibya na al-Zawiya.

Bwana Kobler amesema kwamba mauaji hayo ya raia ni ukiukwaji wa sheria ya kimataifa ya kibinadamu na haki za binadamu.

Taarifa iliyotolewa na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Libya UNSMIL imeeleza kwamba vikundi vilivyojihami vimeripoti kuteka nyara wanaume kadhaa, kuwaua, pamoja na kuua na kujeruhi raia wengine wakiwemo watoto.

Maisha ya wakimbizi wa Mali nchini Burkina Faso hatarini

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula WFP na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuhudumia Wakimbizi UNHCR zimeonya kwamba maisha ya wakimbizi wa Mali 31,000 waliotafuta hifadhi nchini Burkina Faso yatakuwa hatarini iwapo hawataendelea kupewa msaada wa kibinadamu wa dharura.

Mkuu wa WFP nchini Burkina Faso ameeleza kwenye taarifa iliyotolewa leo kwamba wengi wa wakimbizi wanaoishi kambini wanategemea misaada ya kibinadamu tu kwa chakula na mahitaji yao ya msingi, akitegemea hali kuzorota zaidi wakati msimu wa mwambo ukikaribia.