UNAMA yatiwa hofu na kamatakamata ya wanawake na wasichana kwa kutovaa Hijab Afghanistan
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Misaada nchini Afghanistan UNAMA leo umesema una wasiwasi mkubwa kuhusu kukamatwa kiholela na kuzuiliwa kwa wanawake na wasichana kunakofanywa na maafisa wa serikali ya Afghanistan kwa sababu ya madai ya kutofuata kanuni za mavazi ya Kiislamu.