Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Madaktari wa upasuaji wa wakimfanyia upasuaji mgonjwa katika hospitali ya Al-Quds huko Gaza. (Maktaba)
WHO

Kuzuiwa kwa timu za misaada ni tishio la karibuni kwa hospitali za Gaza: OCHA

Kitendo cha kukataa mara kwa mara kwa mamlaka za Israel kuruhusu timu za misaada za Umoja wa Mataifa kupeleka misaada ya kibinadamu inayohitajika sana ndani ya Gaza kumezizuia hospitali tano za kaskazini mwa Gaza kupata "vifaa na vitendea kazi vya kuokoa maisha", imeonya leo ofisi ya Umoja wa Mataifa ya  kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura OCHA. 

Kampuni ya Yvette Amuli, (pichani) iitwayo Kiyana ni miongoni mwa wanufaika wa mradi wa kampuni ndogo na za kati, SME's unaoendeshwa kwa pamoja kati ya Benki ya Dunia na UN Women kwa ushirikiano na Sowers of New Hope, huko Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu…
UN/ Byobe Malenga

Asilimia 40 ya nchi za kipato cha chini zitakuwa maskini zaidi kuliko kabla ya COVID-19

Benki ya Dunia kupitia ripoti ya matarajio ya uchumi kwa mwaka huu wa 2024 inaeleza kuwa baada ya uchumi wa mwaka 2023 kufanya vibaya, nchi za kipato cha chini zitakua kwa 5.5%, chini ya ilivyotarajiwa na kwamba kufikia mwisho wa 2024, karibu 25% ya nchi zinazoendelea na karibu 40% ya nchi za kipato cha chini zitakuwa maskini kuliko kabla ya janga la COVID-19.