EmpowerU Cash+ yabadilisha maisha katika Wilaya ya Lamwo nchini Uganda
Mpango huo wa EmpowerU Cash+ ulikuwa unalenga idadi ya juu ya watoto kufikia wanne kwa kila kaya na kila mtoto kila mwezi alipewa Shilingi 45,000 za Uganda sawa na takribani dola 11 za kimarekani hiyo ikimaainisha kila kaya ilipata jumla ya Shilingi za Uganda 180,000 sawa na takribani dola 47 za kimarekani kwa mwezi. Huduma hiyo ilikuwa kwa muda wa miezi sita katika wilaya za Lamwo, Adjumani, Yumbe, na Obongi lakini hapa ninaangazia wilaya moja tu, Lamwo.