Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Jane Aciro wa kijiji cha Panyule – Agoro akipokea fedha kupitia mpango wa uhawilishaji fedha na UNICEF.
UNICEF/Maria Wamala

EmpowerU Cash+ yabadilisha maisha katika Wilaya ya Lamwo nchini Uganda

Mpango huo wa EmpowerU Cash+ ulikuwa unalenga idadi ya juu ya watoto kufikia wanne kwa kila kaya na kila mtoto kila mwezi alipewa Shilingi 45,000 za Uganda sawa na takribani  dola 11 za kimarekani hiyo ikimaainisha kila kaya ilipata jumla ya Shilingi za Uganda 180,000 sawa na takribani dola 47 za kimarekani kwa mwezi. Huduma hiyo ilikuwa kwa muda wa miezi sita katika wilaya za Lamwo, Adjumani, Yumbe, na Obongi lakini hapa ninaangazia wilaya moja tu, Lamwo. 

Sauti
4'45"
Msichana mdogo amelazwa katika hospitali ya Al-Quds huko Gaza.
© UNICEF/Eyad El Baba

Hali ya Gaza ni zahma juu ya zahma: Mashirika ya UN

Mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yameeielezea hali inayoendelea Gaza siku 105 baada ya kuzuka vita mpya baina ya wapiganaji wa Hamas na vikosi vya Israel, kuwa ni zahma juu ya zahma. Watu zaidi ya milioni 1.7 wametawanywa huku hofu ya milipuko ya magonjwa, janga la njaa na vifo zaidi likitawala.

Sauti
2'
Dkt. Venance Shillingi, Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu Mzumbe nchini Tanzania akizungumza na Idhaa ya Umoja wa Mataifa kando mwa mkutano wa UN na wanazuoni uliofanyika New York, kuanzia Desemba 5-7 2023.
UN/Assumpta Massoi

Ni kwa vipi mfumo wa wamasai kujikwamua unaweza kuwa mfano kwa wengine Afrika?

Kitendo cha kabila la jamii ya wamasai kuweza kujimudu na maisha hata baada ya ukame uliosababishwa na mabadiliko ya tabianchi kuvuruga upatikanaji wa malisho kwa ajili ya mifugo yao kimeonekana kama moja ya mbinu mujarabu zinazoweza kusaidia nchi za Afrika kujengea mnepo wananchi wapo pindi mbinu walizozoea kujipatia kipato zinapovurugika.

Mama kutoka Sudan na watoto wake wanapata hifadhi katika mji wa Chad katika mpaka wa Darfur nchini Sudan.
© UNICEF/Annadjib Ramadane Maha

Uchunguzi wa ukiukwaji mkubwa wa haki na uhalifu Sudan unaendelea: Chande Othman

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kutafuta ukweli nchini Sudan umeanza kazi yake kwa ujumbe wa awali kuwasili mjini Geneva wiki hii, ukizitaka pande zinazozozana nchini Sudan kumaliza mzozo wa kivita nchini humo, kutekeleza wajibu wao wa kulinda raia na kuhakikisha kwamba wahusika wa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu na uhalifu wanawajibishwa.

Wakazi wa kambi ya wakimbizi wa ndani ya Bulengo jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wakiwa kwenye tamasha la mpira wa soka lililoandaliwa na Shirikisho la Soka barani Afrika, na kufanikishwa na WFP.
© WFP/Michael Castofas

Afcon: Shamrashamra zagubikwa na ukimbizi na njaa mashariki mwa DRC

Huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC shamrashamra za mashindano ya Kombe la Mataifa Afrika, Afcon yanayoendelea huku Côte d'Ivoire zinagubikwa na ukimbizi na ongezeko la matukio ya ukatili wa kingono huku shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP likichukua maamuzi magumu kutokana na ukata unaokabili operesheni zake. 


 

Malori yaliyosheheni msaada wa kibinadamu yakijiandaa kuingia Gaza kupitia kivuko cha Rafah. (Maktaba)
© UNICEF/Eyad El Baba

Habari kwa ufupi: Gaza; Sudan; Watoto Ulaya na Asia ya kati

Hii leao mashirika ya Umoja wa Mataifa yamerejea kupaza sauti kuhusu misaada muhimu ya kibinadamu kuendelea kuruhusiwa kuingia Gaza, lile la kuratibu Misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura OCHA likisema kwa mara ya kwanza dawa kwa ajili ya mateka wa Israel zimeripotiwa kuruhusiwa kuingia leo sanjari na msaada kwa ajili ya Wapalestina kwa makubaliano maalum yaliyowezeshwa na serikali za Qatar na Ufaransa.