Mchango wa wanawake katika ushirikiano wa kimataifa watambuliwa
Ikiwa leo ni ni siku ya kimataifa ya wanawake katika ushirikiano wa kimataifa Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi ya Utamaduni, UNESCO Audrey Azoulay amesema kujenga usawa kupitia ushirikiano wa kimataifa kunamaanisha, kutambua nafasi ya wanawake wanaojihusisha na ushirikiano wa kimataifa,na kuwafanya wao chanzo cha hamasa kwa wale wote wanaotaka kushiriki katika mabadiliko hayo.