Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wanawake viongozi wa nchi na serikali wakiwa kwenye picha ya pamoja na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa baada ya kushirilki mkutano wa viongozi wanawake chini ya UNGA77
Steven Viju Philip

Mchango wa wanawake katika ushirikiano wa kimataifa watambuliwa

Ikiwa leo ni ni siku ya kimataifa ya wanawake katika ushirikiano wa kimataifa Mkurugenzi Mkuu wa shirika la  Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi ya Utamaduni, UNESCO Audrey  Azoulay amesema kujenga usawa kupitia ushirikiano wa kimataifa kunamaanisha, kutambua nafasi ya wanawake wanaojihusisha na ushirikiano wa kimataifa,na kuwafanya wao chanzo cha hamasa kwa wale wote wanaotaka kushiriki katika mabadiliko hayo.

Mgonjwa akipatiwa huduma katika chumba cha upasuaji kwenye hospitali ya Al-Quds Gaza
© WHO

Hali si hali hospitali tatu zilizoko Gaza Kaskazini, wajawazito wabebwa kwa machela

Zaidi ya siku 100 za mapigano makali baina ya Israel na wanamgambo wa kipalestina, Hamas pamoja na vikundi vingine vilivyojihami huko ukanda wa Gaza, Mashariki ya kati yaliyoanza tarehe 7 mwezi Oktoba mwaka huu, yamesababisha sio tu vifo miongoni mwa wapalestina na waisraeli bali pia kudhoofika kwa mifumo ya afya, halikadhalika uhaba wa misaada muhimu ya kiutu kama vile chakula, maji, huduma za kujisafi na malazi. Hali imekuwa ya kusikitisha zaidi kaskazini mwa Gaza ambako wakazi walipatiwa amri ya kuhama na mashambulizi yakaelekezwa humo. 

Watoto wakicheza mbele ya kituo cha polisi huko Gao ambacho kilishambuliwa na magaidi.
UN Photo/Marco Dormino

Afrika imekuwa kitovu cha ugaidi duniani: Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 10 wa Umoja wa Mataifa wa kamati Kamati ya Kuratibu Mkataba wa Kimataifa wa Kupambana na Ugaidi barani Afrika katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, jijini New York, Marekani, amesema, "taharuki hii inayoongezeka inateketeza mamilioni ya Waafrika. Hii inajumuisha wanawake na wasichana, ambao wako katika hatari kubwa ya unyanyasaji wa kijinsia na kikatili. Katika bara zima, Da'esh, Al-Qaida na washirika wao wanatumia mienendo ya migogoro ya ndani na udhaifu ili kuendeleza ajenda zao, huku wakisambaratisha mfumo wa kijamii wa nchi nzima na machafuko, kutoaminiana na hofu.”

Makazi ya wakimbizi ya Kyangwali yaliyoko wilaya ya Kikuube magharibi mwa Uganda.
UN News

Makazi ya wakimbizi Uganda yatumia elimu kusongesha amani miongoni mwa wakimbizi

Nchini Uganda katika makazi ya wakimbizi ya Kyangwali wilaya ya Kikuube magharibi mwa taifa hilo, suala la mchango wa elimu kwenye amani liko dhahiri kwani tulipotembelea katika makazi hayo, Yahya Kato ambaye ni Mwalimu Mkuu katika Shule ya msingi Kasonga kwenye makazi hayo ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na Sudan anazungumzia kile wanachofanya. 

Sauti
1'15"
Wanafunzi katika shule moja ya msingi mashariki mwa Nigeria wakisubiri mwalimu aingie masomo yaanze.
© UNICEF/Mackenzie Knowles-Cour

Siku ya Kimataifa ya Elimu 2024 yatumika kukabiliana na kauli za chuki

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limeyatumia maadhimisho ya mwaka huu ya Siku ya Kimataifa ya Elimu kuangazia jukumu muhimu la elimu na walimu katika kukabiliana na kauli za chuki, jambo ambalo limekithiri katika miaka ya hivi karibuni kutokana na matumizi ya mitandao ya kijamii na hivyo kuharibu muundo wa jamii kote duniani. 

Sauti
2'10"