Hedhi salama: UNICEF Kenya yafanikisha utengenezaji wa sodo za kufuliwa
Shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, nchini Kenya limeleta tija kwa wasichana kwa kuwapa sodo za kufuliwa zinazoweza kutumika tena na tena. Kutokana na hilo sasa idadi ya wasichana wanaokosa kwenda shule wakiwa hedhini inaripotiwa kupungua.