Wasudan wangapi wafe ndio pande kinzani Sudan ziache kupigana? Ahoji Türk
Nimeshtushwa sana, kwa mara nyingine na ripoti za muaji ya kikatili ya raia kwenye kijiji cha Wad Al-Noura jimboni al Jazira nchini Sudan, Ndivyo ilivyoanza taarifa ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa haki za binadamu Volker Türk iliyotolewa leo Geneva, USwisi ikijielekeza kwenye tukio hilo la Jumatano lililosababisha vifo vya watu zaidi ya 100.