Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja huo wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO wakiwa kwenye doria katika kijiji cha Logo mji wa Djugu jimboni Ituri .
MONUSCO

Walinda amani wa UN waweka doria kali mashariki mwa DRC baada ya kuibuka mapigano

Katika kukabiliana na hali ya mapigano makali yaliyoibuka tena mwishoni mwa wiki kati ya kundi lenye kujihami kwa silaha M23 na Jeshi la DR Congo (FARDC), walinda amani wa Umoja wa Mataifa kwa uratibu wa FARDC, wameweka doria karibu na Kanyabayonga kusaidia baadhi ya wanaume, wanawake na watoto 150,000 waliokimbia makazi yao katika siku za hivi karibuni mashariki mwa nchi.

Nyanya ameketi na wajukuu zake watatu waliojeruhiwa kwa mafuriko ya ghafla yalipopiga kijiji chao katika jimbo la Baghlan, Afghanistan.
© UNICEF/Osman Khayyam

Mafuriko ya ghafla Afghanistan ni tishio kubwa kwa watoto: UNICEF

Makumi ya maelfu ya watoto nchini Afghanistan wbado wameathiriwa na mafuriko yanayoendelea, hususan katika majimbo ya kaskazini ya Baghlan na Badakhshan na mkoa wa Ghor magharibi mwa Afghanistan, limesema leo shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF na kukumbusha kuwa mafuriko katika nchi hiyo ya Asia ya Kati yanasababisha tishio la haraka na la kudumu kwa watoto.

Mgonjwa anayeugua kipindupindu akitibiwa Tukombo kaskazini mwa Malawi. (Maktaba)
© UNICEF

Mkutano wa dunia kuhusu afya wakubaliana kuhusu marekebisho ya Kanuni za Afya za Kimataifa

Katika hatua ya kihistoria, Mkutano wa 77 wa Dunia kuhusu Afya (WHA77), ambao ni mkutano wa kila mwaka wa nchi wanachama 194 wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, leo umekubali fungu la marekebisho muhimu ya Kanuni za Afya za Kimataifa (2005) (IHR) na kutoa ahadi madhubuti za kukamilisha ndani yam waka mmoja mazungumzo kuhusu makubaliano juu ya janga la afya la kimataifa ndani ya mwaka, ikiwezekana mapema iwezekavyo.

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yana wasiwasi mpya kuhusu athari za uvutaji sigara kwa vijana.
© Unsplash/Tobias Tullius

Chonde chonde walindeni vijana dhidi ya mbinu za biashara ya tumbaku: WHO

Katika siku ya kupinga matumizi ya tumbaku duniani, shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO na kampuni ya kimataifa ta STOP inayofuatilia masuala ya tumbaku wamezindua wamezindua ripoti "Kuunganisha kizazi kijacho," ripoti inayoangazia jinsi tasnia ya tumbaku na nikotini husanifu bidhaa, kutekeleza kampeni za uuzaji na kufanya kazi kuunda mazingira ya sera ili kuwachagiza vijana wa ulimwengu kuwa waraibu.