Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Picha kutoka maktaba, Katibu Mkuu António Guterres akihutubia waandishi wa habari kuhusu Mashariki ya Kati.
UN Photo/Loey Felipe

Tuhuma nzito dhidi ya UNRWA, Katibu Mkuu UN anena, Mkuu wa UNRWA asihi wafadhili

Umoja wa Mataifa unachukua hatua za haraka kufuatia tuhuma nzito dhidi ya wafanyakazi kadhaa wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada kwa wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA). Uchunguzi wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Uchunguzi wa ndani (OIOS) ulianza mara moja, ameeleza Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres kupitia taarifa iliyosambazwa na Msemaji wake usiku wa saa sita Jumapili Januari 28 saa za Marekani.

Kambi ya maangamizi ya Auschwitz-Birkenau kusini mwa Poland
Unsplash/Jean Carlo Emer

Kamwe hatutowasahau wahanga wa mauaji ya maangamizi makubwa ya Holocaust: Guterres

Katika siku ya kimataifa ya kumbukumbu ya mauaji ya maangamizi makubwa ya Holocaust Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres, kupitia ujumbe maalum wa siku hii amesema " leo  tunawaomboleza watoto milioni 6 wa Kiyahudi, wanawake, na wanaume waliouawa katika mikono ya Manazi na washirika wao, na tunawaenzi Waroma na Wasinti, watu wenye ulemavu, na wengine wengi sana ambao waliteswa na kuuawa katika Maangamizi Makubwa ya Holocaust. 

Msichana mwenye umri wa miaka 11 ameketi kwenye vifusi vya nyumba huko Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza.
© UNICEF/Eyad El Baba

Guterres atambua uamuzi wa ICJ kuhusu Gaza, sasa kuwasilisha notisi Baraza la Usalama

Muda mfupi baada ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ huko The Hague, Uholanzi kupitisha uamuzi wa kuitaka Israel pamoja na mambo mengine ichukue hatua zote chini ya uwezo wake wote ku kuepusha mauaji ya kimbari dhidi ya wapalestina huko Ukanda wa Gaza na kuhakikisha misaada ya kiutu inaingia, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametambua uamuzi huo. 

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa IOM, Amy Pope, (mwenye skafu ya buluu) akizungumza na wanawake wa Somalia wakati wa ziara yake ya siku  nne nchini humo.
IOM

Hali ya kutisha ya zaidi ya watu milioni 10 waliokimbia makazi yao kutokana na mizozo nchini Sudan isipuuzwe - IOM

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, IOM Amy Pope amesema hali ya kutisha inayokumba zaidi ya watu milioni 10 waliofurushwa kwenye makazi  yao nchini Sudan kutokana na mapigano haipaswi kupuuzwa. Taarifa ya IOM iliyotolewa leo Geneva, Uswisi na Port Sudan nchini Sudan imemnukuu akieleza kwamba watu milioni 10.7 sasa wamekimbia makazi yao kutokana na migogoro nchini Sudan, na kati yao hao, milioni tisa wamo  ndani ya nchi hiyo kulingana na takwimu mpya kutoka IOM. 

Sala na muda wa ukimya katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kumbukumbu ya Umoja wa Mataifa ya Kuwakumbuka Wahanga wa Mauaji ya Holocaust.
UN Photo/Manuel Elías

Mauaji ya mangamizi: Hakuna jamii iliyo salama dhidi ya ubaguzi

Kuelekeea siku ya kumbukumbu ya waliofariki katika mauaji ya maangamizi makubwa au Holocaust dhidi ya wayahudi hapo kesho 27 Januari Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amekumbusha kuwa mauaji hayo yaliyoanza mwaka 1941- 1945 yalitanguliwa na maelfu ya miaka ya ubaguzi, watu kufukuzwa, kuhamishwa na kuangamizwa na kwamba vitendo kama hivyo sasa vinaenea ulimwenguni.