GAZA: Vita ikishika kasi, uchunguzi wa madai dhidi ya UNRWA ukiendelea, wito watolewa wagaza waendelee kusaidiwa
Mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa leo yameonya kwamba wakati mashambulizi ya Israel yakiendelea kushika kasi Gaza kwa njia ya anga, ardhini na baharini hususan katika mji wa Kusini wa Khan Younis, makazi ya wakimbizi wa ndani yamejaa pomoni mara nne ya uwezo wake na chakula hakitoshi.