OCHA: Hali ya ustawi na usalama bado ni tete kwa raia nchini Sudan
Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura OCHA hii leo imetoa taarifa mpya kuhusu hali ya vita huko nchini Sudan amabapo imeeleza kuwa na wasiwasi mkubwa kuhusu ustawi na usalama wa raia wanaokabiliwa na mapigano makali yanayoendelea katika eneo la Al Fasher, lililoko katika mji mkuu wa Jimbo la Darfur Kaskazini mwa Sudan.