Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hatua za haraka zinahitajika kwa ajili ya kukabiliana na suala la utapiamlo Afrika Magharibi na Kati.
UNICEF/UN0594520/Dejongh

Zaidi ya watoto milioni 6 wako hatarini kwa utapiamlo Sahel:UN 

Mwaka huu wa 2022, takriban watoto milioni 6.3 wenye umri wa miezi 6 hadi miezi 59 katika nchi 6 za ukanda wa Sahel wataathirika na tatizo la uzito mdogo ikilinganishwa na urefu wao na hivyo kuweka maisha ya watoto wasiopungua 900,000 hatarini, linaonya kundi la wataalamu wa kufuatilia lishe katika nchi zilizoko Afrika Magharibi na Kati.  

Taswira ya ukumbi wa Baraza la Usalama la UN wakati Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy (kwenye skrini) alipohutubia  05 Aprili 2022
UN /Loey Felipe

Rais wa Ukraine ataka Baraza la Usalama liungane kwa ajili ya amani

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy amehutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa hisia kali akielezea kwa kinagaubaga kile alichodai kuwa ni mauaji ya makusudi yaliyofanywa na  majeshi ya Urusi dhidi ya raia huko Bucha, viungani mwa mji mkuu Kyviv, hotuba ambayo ametoa huku akitaka wajumbe wa Baraza kuchagua kuhusu  hatma ya muundo wa ulinzi na usalama ulioanzishwa baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia.