Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Sedelia Abdullahi ni mhudumu wa afya wa mstari wa mbele huko mashinani nchini Ethiopia na kila siku huchunguza na kutibu watoto wenye utapiamlo kwenye kituo cha afya cha kambi ya wakimbizi ya Bambassi nchini Ethiopia kilichojengwa na UNICEF kwa ufadhili …
UNICEF Ethiopia

Wahudumu wa afya Ethiopia warejesha tabasamu kwa watoto- UNICEF

Nchini Ethiopia, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniain, UNICEF kupitia msaada kutoka Muungano wa Ulaya umewezesha mamia ya wahudumu wa afya walio mstari wa mbele kila uchao kuweza kutembelea wakimbizi wa ndani waliofurushwa makwao kutokana na mzozo kwenye jimbo la Benishangul-Gumuz lililoko kaskazini-magharibi mwa taifa hilo, likipakana na Sudan ili kuwapatia huduma za lishe bora wakati huu ambapo watoto wanakabiliwa na utapiamlo.

Sauti
2'31"
Taswira ya ukumbi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
UN Photo/Manuel Elías

UNGA77 yafunga pazia, Afrika yasema sasa ni wakati wa kuwa na ujumbe wa kudumu

Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA77 umekunja jamvi kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa ukiwa na maudhui: Wakati muhimu: Majawabu ya kuleta marekebisho kwa changamoto zinazofungamana. Katika siku 6 za mjadala huo nchi za Afrika zilitumia fursa kuhoji marekebisho gani yanawezekana bila kurekebisha chombo hicho ambacho kura  yenye maamuzi ya msingi inamilikiwa na wanachama 5 kati ya 193, ikiwa ni miaka 77 tangu kuudwa kwake.