Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNGA77

MKUTANO WA 77 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Pata habari kutoka UNGA77

Mambo sasa yameiva kwa ajili ya Mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Wakati dunia inaanza taratibu kujikwamua kutoka katika janga baya kabisa la COVID-19, mjadala wa ngazi ya juu wa mkutano wa 77 kwa kiasi kikubwa utafanyika kwa viongozi kuweko kwenye ukumbi mashuhuri wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, tofauti ya miaka miwili iliyopita ambapo viongozi wengine walikuweko ukumbini na wengine walitoa hotuba zao kwa njia ya video. 
 
Katika ukurasa huu, Habari za UN itakupatia kiti cha mbele kabisa kutoka kwenye kumbi zote. Kupitia simu yako ya kiganjani au rununu bila kusahau kompyuta yako au kishkwambi, utafuatilia hotuba za wakuu wa nchi na serikali wakati wakitoa ainisho au majawabu ya changamoto zinazokabili Dunia hivi sasa, sambamba na wanavyoshiriki katika mkutano wa ngazi ya juu wa Marekebisho ya Mfumo wa Elimu, kushughulikia janga la chakula duniani, maadhimisho ya miaka 30 ya Azimio la UN kuhusu haki za watu wa makabila madogo halikadhalika mzozo wa Ukraine.

Rambaza kwenye majukwaa yetu ya mitando ya kijamii

Twitter: Habari za UN
Youtube: Habari za UN

Csaba Kőrösi (kushoto) Rais wa mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la UN akikabishi rungu la kuongoza mkutano kwa Rais wa mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la UN (UNGA78). Kulia kabisa ni Naibu Katibu Mkuu wa UN Amina J. Mohammed
UN /Manuel Elias

UNGA 77 yafunga pazia, Rais wa UNGA78 ala kiapo

Mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umekunja jamvi asubuhi ya tarehe 5 Septemba 2023, jijini New York, Marekani kwa Rais wa mkutano huo anayemaliza muda wake Csaba Kőrösi akisisitiza kuwa licha ya mikingamo ya kijiografia, ushirikiano baina ya nchi haukwepeki.

06 OKTOBA 2022

Hii leo katika Habari za UN Assumpta Massoi anakuletea Habari kwa Ufupi, Mada kwa Kina na Kujifunza Lugha ya Kiswahili.

Katika Habari kwa Ufupi kuna haki za mtoto kuzingatiwa hasa wakati huu ambapo majanga ya kiasili na yanayosababishwa na binadamu  yanakengeua utekelezaji wa haki za mtoto. Suala la afya ya akili barani Afrika ambayo inachochea matukio ya kujiua ,na WHO imezindua kampeni maalum. Na kisha ni uzinduzi wa ripoti kuhusu matumizi ya matukio makubwa ya michezo ili kuimarisha afya ya mwili ya binadamu.

Sauti
11'26"
Csaba Kőrösi  Rais wa UNGA77 akiendesha mjadala wa wazi wa Baraza Kuu katika siku ya mwisho ya mjadala huo
UN Photo/Cia Pak

Körösi, akunja jamvi la mjadala wa ngazi ya juu wa UNGA77

Magari yaliyotanda kuzunguka makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kuhakikisha usalama wakati wa wiki ya mjadala wa ngazi ya juu wa viongozi kwenye Baraza Kuu UNGA77 sasa yameondoka na barabara iliyofungwa kufunguliwa, polisi wengi na maafisa wa ujasusi ambao walizuia njia za kuelekea kwenye jengo la Umoja wa Mataifa, nao wametrejea kwenye majukumu yao ya kila siku, kilomita za vyuma vilivyokuwa vizuizi kuzunguka eneo hilo la Umoja wa Mataifa New York, vinavyojulikana kama Turtle Bay navyo vimesafirishwa kwa malori hadi kwenye maghala kusubiri hadi mwakani kwani wiki ya mjadala wa ngazi ya juu imemalizika kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa  .

Taswira ya ukumbi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
UN Photo/Manuel Elías

UNGA77 yafunga pazia, Afrika yasema sasa ni wakati wa kuwa na ujumbe wa kudumu

Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA77 umekunja jamvi kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa ukiwa na maudhui: Wakati muhimu: Majawabu ya kuleta marekebisho kwa changamoto zinazofungamana. Katika siku 6 za mjadala huo nchi za Afrika zilitumia fursa kuhoji marekebisho gani yanawezekana bila kurekebisha chombo hicho ambacho kura  yenye maamuzi ya msingi inamilikiwa na wanachama 5 kati ya 193, ikiwa ni miaka 77 tangu kuudwa kwake.

27 Septemba 2022

Hii leo katika Habari za UN Flora Nducha anakuletea Habari kwa Ufupi, Mada kwa kina na Mashinani.

Katika Habari kwa ufupi: Kurejea nyumbani kwa hiyari kwa wakimbizi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kutoka nchini Zambia. Pili kutangazwa kutokomezwa kwa EBola nchini DRC na Habari ya Tatu ni kuhusu siku ya utalii duniani na wito kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa kutaka utalii wa aina mpya usioaharibu mazingira na wenye mnepo kwa kila mkazi wa dunia.

Sauti
13'48"