Dola milioni 818 zinahitajika kutoa huduma muhimu na za kuokoa maisha kwa wanawake na wasichana walioathiriwa na mizozo-UNFPA
Shirika la idadi ya watu la Umoja wa Mataifa, UNFPA, leo limezindua ombi lake kubwa kuliko yote la msaada wa kibinadamu.
Shirika la idadi ya watu la Umoja wa Mataifa, UNFPA, leo limezindua ombi lake kubwa kuliko yote la msaada wa kibinadamu.
Kutana na mkimbizi kutoka Syria ambaye sasa anaishi kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani ya Atma iliyoko karibu na mpaka wa Uturuki. Pamoja na madhila yote aliyopitia anapata faraja anapoweza kubadili maisha japo ya mkimbizi mmoja kwa ushauri nasaha anaotoa kwa maelfu ya wakimbizi kambini hapo
Shirika lisilo la kiserikali la CAMFED nchini Tanzania linaendeleza harakati za kutetea haki za watoto, hususani wa kike, kuwaondoa kwenye ajira za utotoni na kusaidia kuwarejesha shuleni. John Kabambala wa redio washirika KidsTime FM ya Morogoro amewahoji wadau wa shirika hilo.
Wakati Tanzania ikijiandaa kupeleka kikosi chake katika vikundi vipya vitakavyokuwa na uwezo wa kuchukua hatua haraka zaidi kukabiliana na vitisho na hatimaye kuimarisha ulinzi wa raia nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC , chini ya bendera ya Umoja wa Mataifa, mkuu wa mafunzo na utendaji wa kivita wa jeshi la wananchi wa Tanzania, JWTZ amezungumzia kile ambacho watafanya ili utendaji wao uendane zaidi na mazingira. Tupate maelezo zaidi kutoka Luteni Issa Mwakalambo Afisa habari wa kikosi cha 7 cha Tanzania kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi. FIB, cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO.
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya wafanyakazi wa kujitolea, Umoja wa Mataifa umetumia siku hii adhimu kuangazia wafanyakazi wa kujitolea na mchango wao katika kukabiliana na ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona au COVID-19.
Katika kuelekea siku ya udongo duniani hapo kesho Desemba 5 shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO limesema bayonuai ya udongo ina jukumu muhimu la kuchagia katika uzalishaji wa chakula , kuimarisha lishe, kulinda afya ya binadamu, kupunguza uchafuzi wa mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi , lakini mchango wake mara nyingi haupewi uzito unaostahili.
Shirika la Mpango wa Chakula la Umoja wa Mataifa, WFP limekaribisha kusainiwa kwa makubaliano ili kuwezesha upatikanaji wa huduma za kibinadamu ambazo hazina kizuizi, endelevu na salama kwa maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa Serikali ya Shirikisho katika mkoa wa Tigray na maeneo yanayopakana na mikoa ya Amhara na Afar.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, liko tayari kuanza tena shughuli zake kamili za kibinadamu katika mkoa wa Tigray, Ethiopia mara tu hali itakaporuhusu, kufuatia makubaliano ya kurejesha upatikanaji, ameeleza hii leo msemaji wa shirika hilo Babar Baloch katika mkutano wake na vyombo vya habari mjini Geneva Uswisi.
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO limesema mlipuko mpya wa homa ya manjano nchini Nigeria umeshakatili maisha ya watu 172 na wengi 530 wanashukiwa kuambukizwa homa hiyo.
Hoja ya umuhimu wa kutunza bayonuai ya udongo, ambayo ni maudhui ya siku ya udongo duniani, inayoadhimishwa tarehe 5 mwezi desemba mwaka huu ni moja ya mafunzo waliyopatiwa wakulima wawezeshaji nchini Tanzania.