Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Walinda amani kutoka Tanzania na Indonesia wakikagua daraja.
TANZBATT 7/Ibrahim Mayambua

Tumejipanga ili kutoa mchango bora zaidi katika vikundi vipya vya ulinzi wa amani DRC- Meja Jenerali Kapinga

Wakati Tanzania ikijiandaa kupeleka kikosi chake katika vikundi vipya vitakavyokuwa na uwezo wa kuchukua hatua haraka zaidi kukabiliana na vitisho na hatimaye kuimarisha ulinzi wa raia nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC , chini ya bendera ya Umoja wa Mataifa, mkuu wa mafunzo na utendaji wa kivita wa jeshi la wananchi wa Tanzania, JWTZ amezungumzia kile ambacho watafanya ili utendaji wao uendane zaidi na mazingira. Tupate maelezo zaidi kutoka Luteni Issa Mwakalambo Afisa habari wa kikosi cha 7 cha Tanzania kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi. FIB, cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO. 

Sauti
4'13"
Wanafunzi wakimwagilia mimea maji kwenye shule ya msingi Laos.
© FAO/Manan Vatsyayana

Bioanuwai ya udongo ina umuhimu mkubwa lakini mchango wake haujapewa uzito unaostahili-FAO 

Katika kuelekea siku ya udongo duniani hapo kesho Desemba 5 shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO limesema bayonuai ya udongo ina jukumu muhimu la kuchagia katika uzalishaji wa chakula , kuimarisha lishe, kulinda afya ya binadamu, kupunguza uchafuzi wa mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi , lakini mchango wake mara nyingi haupewi uzito unaostahili. 

Wakimbizi waliowasili kutoka Tigray Ethiopia wakileta msaada kwa ajili ya kukarabati makazi kambi ya Raquba, Kassal, Sudan.
UNFPA/Sufian Abdul-Mouty

Tigray Ethiopia, WFP yatangaza kipaumbele chake

Shirika la Mpango wa Chakula la Umoja wa Mataifa, WFP limekaribisha kusainiwa kwa makubaliano ili kuwezesha upatikanaji wa huduma za kibinadamu ambazo hazina kizuizi, endelevu na salama kwa maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa Serikali ya Shirikisho katika mkoa wa Tigray na maeneo yanayopakana na mikoa ya Amhara na Afar.