UN yatoa ombi la dola bilioni 1 kwa ajili ya mfuko wa dharura CERF
Umoja wa Mataifa umesema mfuko wa dharura wa Umoja huo CERF mwaka huu wa 2020 umetoa dola milioni 820 kwa ajili ya msaada wa kifedha kwa nchi 52 kote duniani.
Umoja wa Mataifa umesema mfuko wa dharura wa Umoja huo CERF mwaka huu wa 2020 umetoa dola milioni 820 kwa ajili ya msaada wa kifedha kwa nchi 52 kote duniani.
Huko jimboni Darfur nchini Sudan , walinda amani kutoka Tanzania kwenye ujumbe wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika wa kuweka utulivu jimboni Darfur, (UNAMID) wamekabidhi kwa wakazi wa Khor Abeche jengo jipya la madrasa.
Mkurugenzi wa Huduma ya Habari ya Umoja wa Mataifa Alessandra Vellucci, akijibu maswali ya wanahabari hii leo mjini Geneva Uswisi, amesema kwamba Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ana wasiwasi kuhusu hali ya sasa katika mkoa wa Tigray nchini Ethiopia.
WHO leo imezindua kampeni ya mwaka mzima kwa jina "Jitolee kuacha kuvuta." kwa ajili ya maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kutovuta tumbaku kwa mwaka ujao wa 2021.
Wakati huu dunia ikiendelea kuhaha kuhakikisha chanjo dhidi ya corona au COVID-19 iliyokwishapatikana inasambazwa kwa kila mkazi wa dunia, shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO limefafanua kuhusu chanjo na jinsi zinavyotengenezwa.
Ukosefu wa usawa wa jinsia, ugumu wa kupata huduma na umaskini vinaripotiwa kuchochea kiwango kikubwa cha mimba za utotoni na na virusi vya Ukimwi VVU huko Homa Bay nchini Kenya. Taarifa hizo ni kwa mujibu wa ripoti mpya iliyoandaliwa na serikali ya kaunti ya Homa Bay kwa kushirikiana na wadau wake kupitia msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.
Idadi ya watoto wa shule walioathiriwa na kufungwa kwa shule kutokana na janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 imeongezeka kwa asilimia 38 mwezi uliopita wa Novemba, hali hiyo ikiweka mkwamo mkubwa kwenye maendeleo ya masomo na ustawi wa wanafunzi zaidi ya milioni 90 ulimwenguni, limeeleza shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF.
Tukiwa bado na siku 16 za harakati za kupinga uakatili wa kijinsia dhidi ya wanawake, leo tunamulika mwanaharakati wa haki za binadamu kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC , Francoise Sabuni Chikunda ambaye amepitia madhila yasiyoelezeka, ikiwemo kubakwa na hata familia yake kuuawa, lakini yote hayo hayakumkatisha tamaa bali yamempa ujasiri wa kuwa nuru ya wanawake wakimbizi wenzake katika makazi ya wakimbizi ya Nakivale nchini Uganda.
Harakati za kupunguza na hatimaye kuondoa kabisa vikosi vya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO umekuwa ukiendelea sambamba na utekelezaji wa mkakati wa pamoja wa kuhakikisha kuwa hatua hiyo haitaweka ombwe la usalama kwenye taifa hilo la Maziwa Makuu.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limetoa ombi la juu kabisa kuwahi kuombwa na shirika hilo, dola za kimarekani bilioni 2.5 kwa ufadhili wa dharura, taarifa iliyotolewa hii leo mjini Amman Jordan imeeleza.