Mafaniko ya UNISFA yalindwe katika kutatua suala la Abyei-Lacroix
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo Jumanne limekutana jijini New York, Marekani kujadili hali ya Sudan na Sudan Kusini hususan eneo gombaniwa la Abyei.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo Jumanne limekutana jijini New York, Marekani kujadili hali ya Sudan na Sudan Kusini hususan eneo gombaniwa la Abyei.
Muziki wa Jazz unaelezea maisha na una jukumu muhimu la kuchagiza amani, majadiliano na kuyafanya maisha yawe na maana muhimu kwa watu wote duniani, amesema mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu sanyansi na utamaduni UNESCO katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya muziki wa Jazz hii leo.
Nchini Libya maelfu ya wanawake, watoto na wanaume wamelazimika kufungasha virago na kukimbilia nje ya mji mkuu Tripoli kufuatia machafuko yanayoendelea katika eneo la Kaskazini la mji huo.
Wahudumu wa misaada ya kibinadamu wamekuwa wakikimbizana kuwafikishia waathirika wa kimbunga Kenneth msaada wa dharura baada ya mvua kusita kwa muda leo asubuhi mjini Pemba nchini Msumbiji.
Kuendelea kuwepo kwa madeni hususan kwa mataifa yanayoendelea barani Afrika ni moja ya changamoto ambayo inakwamisha maendeleo katikabara hilo.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na mjadala ulioleta pamoja wadau mbalimbali kujadili kuhusu huduma ya afya kwa wote duniani ikiwa ni maandalizi ya mkutano wa ngazi ya juu wa viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhusu mada hiyo mwezi Septemba mwaka huu.
Ofisi ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva Uswisi imefanya kongamano kwa ajili ya kukabiliana na kauli za chuki ili kulinda vikundi vidogo vya kidini, wakimbizi na wahamiaji.
Fedha za msaada zilizotolewa na Umoja wa Mataifa zitasaidia kuhakikisha chakula , malazi, huduma za afya na maji safi vinapatikana kwa waathirika wa kimbunga Kenneth nchini Msumbiji. Nchi hiyo ina watu 18,000 waliotawanywa na kimbunga Kenneth ambao hivi sasa wanapata hifadhi kwenye makazi ya muda. Watu38 wamefariki dunia kufuatia kimbunga hicho kufikia sasa.
Watalaam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wametaka mamlaka zilizoko hivi sasa Yemen kutupilia mbali mara moja adhabu ya kifo aliyohukumiwa Hamid Kamali bin Haydara, kwasababu tu ya kuwa muumini wa dini ya Bahá’í.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema linasaka dola milioni 29 ili kuongeza bajeti yake ambayo kwa sasa ni takribani dola milioni sita tukwa lengo la kuwasaidia maelfu ya Watoto wa Venezuela wanaoishi nchini Colombia.