Mlipuko wa kipindupindu wadhibitiwa miongoni mwa wakimbizi, Uganda
Licha ya idadi ya wakimbizi walioambukizwa maradhi ya kipindupindu nchini Uganda kuongezeka hadi 949 kutoka takribani wagonjwa 700 Ijumaa iliyopita, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR, nchini humo limesema mlipuko huo umeanza kudhibitiwa.