Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katika kituo cha afya cha uzazi Al Sabeen Sana'a Yemen, WFP inatoa lishe iliorutubishwa kutibu mtoto Ali Yakya Ali anayeugua utapiamolo uliokithiti wakati babake akifuatilia. Novemba 2018
WFP/Marco Frattini

Maisha ya watu milioni 20 hatarini kwa tisho la baa la njaa Yemen-UN

Hali mbaya ya uhakika wa chakula inayoongezeka haraka nchini Yemen inaweka rehani Maisha ya karibu watu milioni 20 kwa mujibu wa tathimini ya uhakika wa chakula (IPC) iliyotolewa leo na serikali ya Yemen, Umoja wa Mataifa washirika wa misaada ya kibinadamu.Shirika la mpango wa chakula duniani WFP limesema msaada wake wa chakula ndio msaada pekee unaoepusha janga kubwa la baa la njaa nchini humo lakini mapigano yanayoendelea, kupanda kwa beiza vyakula na kuporomoka kwa uchumi viwanawasukuma watu kuelekea kwenye baa la njaa.

Wasaka hifadhi wakiokolewa na meli ya ubelgiji katika bahari ya mediteranea
Frontex/Francesco Malavolta

Kigeugeu kwenye mkataba wa kimataifa wa uhamiaji ni taswira mbaya kwa nchi husika:Abour

Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya uhamiaji wa kimataifa  Louise Abour amesema dhamira iliyowekwa bayana na nchi kadhaa ikiwemo Hungary, Poland , Jamhuri ya Czech na Australia ya kujiengua kwenye mkataba wa kimataifa wa wahamiaji inaonyesha picha mbaya kwao na ina athari kubwa katika ari ya ushirikiano wa kimataifa . 

Sauti
3'23"
Millie Bobby Brown akiwa mjini New York wakati wa kutengeneza video ya siku ya mtoto mwaka 2018
UNICEF/UN0248272/Clarke

Leo ni siku kubwa kwa watoto kote duniani.

Wakati dunia ikiadhimisha siku ya mtoto duniani, Millie Bobby Brown ametangazwa kuwa balozi mwema mpya wa Shirika la kuhudumia watoto UNICEF.  Mtoto huyu wa umri wa miaka 14 anakuwa mtu mdogo zaidi kuwa na wadhifa huo wa balozi mwema wa UNICEF.