Maisha ya watu milioni 20 hatarini kwa tisho la baa la njaa Yemen-UN
Hali mbaya ya uhakika wa chakula inayoongezeka haraka nchini Yemen inaweka rehani Maisha ya karibu watu milioni 20 kwa mujibu wa tathimini ya uhakika wa chakula (IPC) iliyotolewa leo na serikali ya Yemen, Umoja wa Mataifa washirika wa misaada ya kibinadamu.Shirika la mpango wa chakula duniani WFP limesema msaada wake wa chakula ndio msaada pekee unaoepusha janga kubwa la baa la njaa nchini humo lakini mapigano yanayoendelea, kupanda kwa beiza vyakula na kuporomoka kwa uchumi viwanawasukuma watu kuelekea kwenye baa la njaa.