Baraza Kuu laidhinisha bajeti ya UN kwa 2020 ni zaidi ya dola bilioni 3
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Ijumaa jioni limeidhinisha bajeti ya Umoja huo kwa mwaka 2020 ambayo ni jumla ya dola 3,073,830,500.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Ijumaa jioni limeidhinisha bajeti ya Umoja huo kwa mwaka 2020 ambayo ni jumla ya dola 3,073,830,500.
Watalaam huru wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa leo wamelaani vikali hukumu ya kifo aliyopewa mhadhiri wa chuo kikuu cha Bahauddin Zakariya nchini Pakistan kwa madai ya kukashifu dini.
Klinini ya mazoezi ya viungo inayotoa huduma bure kwa wakimbizi wa Rohingya na jamii zinazowahifadhi nchini Bangladesh imeleta matumaini mapya kwa pande zote zinazopokea huduma .
Mradi wa serikali ya Brazil na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR wa kuwahamisha wakimbizi umeleta matumaini mapya kwa maelfu ya wakimbizi wa Venezuela walioko mashambani nchini Brazil. Brenda Mbaitsa na taarifa Zaidi
Wigo wa lugha ya Kiswahili unaendelea kupanuka kila uchao na ni kwa mantiki hiyo ambapo watu wengi wanajikuta wakichukua masomo ambayo yanajikita pia na lugha hiyo.
Katika nchi nyingine, usajili wa kuzaliwa haupewi kipaumbele kama jambo la kawaida kufuatia kuzaliwa kwa mtoto. Lakini kwa wengine wengi, ni hatua muhimu inayokosekana katika kuthibitisha utambulisho wa kisheria wa mtoto. Bila huo, watoto hawatambuliki na serikali zao, hivyo haki zao zinaweza kutolindwa na kutozingatiwa, pamoja na huduma muhimu kama huduma za afya na elimu.
Karibu robo ya watoto wote waliozaliwa duniani walio chini ya wa miaka 5 hawajawahi kusajiliwa. Maisha ya watoto hawa ni muhimu, lakini hawawezi kulindwa ikiwa serikali hawatambui.
Mtaalam maalum wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu mauaji na mauaji ya kiholela Agnes Callamard amesema ameshtushwa sana na hukumu ya kifo waliyopewa wanaodaiwa kumuua mwandishi wa Habari wa Saudia Jamal Khashoggi huku walioamuru mauaji hayo wakiachwa bila kuguswa.
Ikiwa imesalia takribani miaka kumi kufikia mwaka 2030 ambao umepangwa kuwa ukomo wa utimizaji wa malengo 17 ya maendeleo endelevu, SDGs ,juhudi kote duniani zinaendelea kuhakikisha lengo hilo linafikiwa.
Kutana na mkimbizi kutoka Syria Mustafa ambaye hii ni mara ya tano amelazimimika kufungasha virago yeye na familia yake ili kunusuru maisha yake. Pamoja n ayote hayo hakati tamaa ya kurejea nyumbani.
Ubakaji unasalia kuwa moja ya uhalifu mbaya zaidi duniani na cha kusikitisha ni kwamba asilimia kubwa ya waathirika hushindwa kujitokeza au kushitaki uhalifu huo wakidhani kuwa ni makosa yao.