Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kiswahili kinazidi kutamba hata vyuoni ikiwemo Chuo Kikuu cha Nairobi Kenya

Chuo Kikuu cha Nairobi anakosemea Nosizi Reuben Wanafunzi wa chuo Kikuu cha Nairobi, kitengo cha tafsiri na ukalimani, Kenya
UN News/Grece Kaneiya
Chuo Kikuu cha Nairobi anakosemea Nosizi Reuben Wanafunzi wa chuo Kikuu cha Nairobi, kitengo cha tafsiri na ukalimani, Kenya

Kiswahili kinazidi kutamba hata vyuoni ikiwemo Chuo Kikuu cha Nairobi Kenya

Utamaduni na Elimu

Wigo wa lugha ya Kiswahili unaendelea kupanuka kila uchao na ni kwa mantiki hiyo ambapo watu wengi wanajikuta wakichukua masomo ambayo yanajikita pia na lugha hiyo.

Mapema mwezi huu nimepata fursa ya kutembelea Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya ili kufahamu mengi zaidi kuhusu kitengo cha tafsiri na ukalimani ambacho tunashirikiana nacho katika kutafsiri baadhi ya kurasa za kazi za Umoja wa Mataifa ambazo utaweza kuzipata kwenye wavuti wetu kupitia news.un.org/sw. Nimezungumza na mhadhiri wao ambaye amenidokezea kuhusu kitengo hicho
(Play clip)

Lakini je wanafunzi wenyewe wanasema nini? tumsikie kwanza Rajab Abdalla kutoka Tanzania ambaye anasomea utafsiri ukijumuisha lugha ya Kiswahili nchini Kenya, kulikoni?

(Play clip)

Kwa upande wake kijana Mary Mukami anatoa ushauri kwa vijana katika mtazamo wao kuhusu Kiswahili

(Play Clip)