Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wanawake wakiwa katika kambi ya wakimbizi wa ndani Sudan. (Maktaba)
© UNOCHA/Ala Kheir

Baraza la usalama saidieni wanawake wa Sudan kupambana na ukatili katika mizozo

Wakati wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wakijiandaa na mjadala wa wazi hapo wiki ijayo kuhusu ukatili wa kijinsia katika maeneo yenye migogoro, wameombwa kutuma ujumbe usio na shaka chini ya sheria ya kimataifa ya kibinadamu kuwa raia wa nchini Sudan lazima walindwe na kamwe wasitendewe vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia ambavyo vinajumuisha uhalifu wa kivita.