Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ukraine

Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa lilikutana Geneva kwa kikao chake cha 55.
UN Photo/Elma Okic

Mkuu wa Umoja wa Mataifa azindua ahadi ya ulinzi wa haki

Mashambulio ya pande zote ya Israel dhidi ya Rafah yatasababisha Umoja wa Mataifa kufikia mwisho wa kutoa misaada ya kibinadamu kwa watu wa Gaza, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameonya hii leo Jumatatu, katika wito wake upana kwa jumuiya ya kimataifa kutekeleza "jukumu lake la msingi."  la kukuza na kulinda haki za binadamu kila mahali na kwa kila mtu.

Kitongoji hiki huko Bucha kiliteseka sana wakati wa uvamizi wa Urusi. Nyumba hii ilipigwa bomu. Leo kila kitu kimerejeshwa kabisa.
UN News/Anna Radomska

Ukraine: Bucha na Irpin zinaibuka kutoka kwenye majivu ya uvamizi wa jeshi la Urusi

Wakati uvamizi wa Urusi huko Bucha katika siku za mwanzo za uvamizi kamili wa Urusi nchini Ukraine, ulimalizika mnamo Machi 2022, uharibifu mkubwa ulionekana, na tume ya Umoja wa Mataifa ikihitimisha kwamba uhalifu wa kivita ulikuwa umetendwa dhidi ya raia, miaka miwili baadaye, maisha yanarudi katika mji ulio nje kidogo ya Kyiv, ambao umerejeshwa kwa msaada wa UN.

Mama na watoto wake wawili wakijinkinga kutokana na mashambulizi ya mabomu katika kituo cha metro cha Kyiv mnamo Januari 2024.
© UNICEF/Aleksey Filippov

Vita nchini Ukraine itaathiri vizazi na vizazi: UN Ripoti

Uvamizi kamili wa Urusi nchini Ukraine, ukiingia mwaka wake wa tatu wiki hii, umesababisha "gharama ya kutisha ya binadamu na mateso makubwa kwa mamilioni ya raia ambayo yatahisiwa na vizazi na vizazi",amesema leo Kamishina Mkuu wa Haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa  mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk.

UNDP inasaidia kutegua mabomu ya ardhini nchini Ukraine.
UNDP in Ukraine/Alexander Ratushnyak

Uondoaji wa mabomu ya kutengwa ardhini Ukraine ni mtihani na hatari kubwa: Paul Heslop

Umoja wa Mataifa umesema Ukraine sasa ni moja ya nchi zilizoathiriwa zaidi na mabomu ya kutegwa ardhini duniani huku ikadiriwa kwamba karibu thuluthi moja ya nchi hiyo imeghubikwa na vita eneo ambalo ukubwa wake ni mara nne na nusu ya nchi ya Uswisi. Umoja wa Mataifa umekuwa ukifanya kazi na serikali ya Ukraine kwa miaka 30 na umekuwa ukiongoza mpango wa utekelezaji wa uteguaji wa mabomu ya kutegwa ardhini tangu 2016. 

Sauti
2'33"