OCHA na wadau waendelea kutoa misaada ya kuokoa maisha Ukraine
Msemaji wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya uratibu wa misaada ya dharura, OCHA Jens Laerke hii leo mjini Geneva Uswisi amesema wakati vita ikiendelea nchini Ukraine, ikiwa na athari mbaya kwa jamii hasa mashariki na kusini, OCHA na wadau wa kibinadamu wanaendelea kuwafikia watu wengi zaidi kwa msaada.