Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Syria

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataif kwa Syria, Geir O.pedersen akizungumza na wanahabari. (PIcha ya maktaba)
UN Photo/Evan Schneider

Nina matumaini na mazungumzo ya jumatano hii kuhusu Syria- Pedersen

Saa chache kuelekea jumatano ya wiki hii ambapo wajumbe wa Kamati ya Katiba ya Syria watakutana kwa mara ya kwanza mjini Geneva Uswisi kujaribu kukubaliana kuhusu Katiba ya nchi hiyo iliyoghubikwa na vita, Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa Geir O.Pedersen amerelejea wito wake wa kusitisha mapigano nchi nzima na kuachiliwa kwa wafungwa ili kujenga kuaminiana kati ya pande zinazokinzana.

Mtoto akipatiwa chanjo ya polio kwa njia ya matone katika kituo cha afya mjini Damascus, Syria
UNICEF/Halabi

Watoto 65,000 wapata chanjo Syria na msaada mwingine licha ya machafuko yanayoendelea:UNICEF/WHO/WFP

Kampeni ya chanjo ya polio iliyokuwa imepangwa hata kabla ya machafuko kushika kasi Kaskazini Mashariki mwa Syria imeendelea bila tukio lolote baya. Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, takriban watoto 65,000 wamepatiwa chanjo hiyo katika jimbo la Hassakeh wakiwemo 1,748 kambini  Al Hol na 740 katika kambi ya Areesheh siku ya Jumatano na Alhamisi wiki hii.