CERF yatoa dola milioni 10 kusaidia waliokimbia Sudan na kuingia Sudan Kusini
Mratibu wa mfuko wa dharura wa Umoja wa Mataifa CERF bwana Martin Griffiths, leo ametangaza kutenga dola milioni 10 kutoka kwenye mfuko huo kwa ajili ya kuwasaidia wanaume, wanawake na watoto wanaokimbia Sudan na kuingia katika nchi jirani ya Sudan Kusini.