Sasa mkataba wa Marrakech ni rasmi, Baraza Kuu la UN laupitisha
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo limepitisha kwa kishindo mkataba wa kimataifa wa uhamiaji salama, wenye mpangilio na unaofuata kanuni za kawaida.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo limepitisha kwa kishindo mkataba wa kimataifa wa uhamiaji salama, wenye mpangilio na unaofuata kanuni za kawaida.
Katika kuadhimisha siku ya uhamiaji duniani hii leo, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM, António Vitorino ametaka hatua zaidi na za dharura zichukuliwe ili kulinda kundi hilo ambalo kila uchwao linakumbwa na madhila kote ulimwenguni.
Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, Baraza Kuu la chombo hicho litapitisha mkataba wa kimataifa wa wakimbizi na hivyo kusaidia kwa kiasi kikubwa wale wanaokimbia makwao na nchi zinazowahifadhi, ambazo mara nyingi ni zile maskini zaidi duniani. Siraj Kalyango na maelezo zaidi.
Mkataba wa kimataifa wa wakimbizi: Tofauti ni ipi na mkataba wa wahamiaji na ni kwa vipi utasaidia watu waliolazimika kukimbia makwao?
Kufuatia kupitishwa hii leo huko Marrakech nchini Morocco, mkataba wa kimataifa kuhusu uhamiaji salama, unaofuata kanuni na wa kawaida, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesema hatua hiyo ya kihistoria ni mafanikio kwa wahamiaji watoto na serikali.
Leo ni siku ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa ikiwa ni tarehe ya kukumbuka kupitishwa kwa azimio la haki za binadamu duniani, UDHR ambalo leo linatimiza miaka 70.
Wakuu wa nchi na serikali, mawaziri, viongozi wengine wa ngazi ya juu, asasi za kiraia na wawakilishi toka sekta za umma na binafsi wamekusanyika mjini Marrakech nchini Morocco, kwa ajili ya mkutano wa ngazi ya juu kwa lengo moja tu, kupitisha mkataba wa kimataifa wa uhamiaji.
Miaka 70 tangu kupitishwa kwa mkataba wa kimataifa wa kuzuia mauaji ya kimbari, bado watu wanauawa, wanabakwa, nyumba zao kutiwa moto, wananyang’anywa ardhi zao kwa sababu tu ya utambulisho wao.
Mkutano wa mwaka wa mfuko wa Umoja wa Mataifa wa usaidizi wa dharura kwa majanga yanayokumba binadamu, CERF umefanyika leo jijini New York, Marekani ambapo Katibu Mkuu wa umoja huo, Antonio Guterres amesema CERF amesihi wahisani kuchangia zaidi ili kufikia lengo la uchangiaji la dola bilioni 1 kwa mwaka lililowekwa na Baraza Kuu la umoja huo miaka miwili iliyopita.
Mila na desturi za kitamaduni zina mchango mkubwa katika jamii endapo zitaenziwa kwa kuheshimu haki zingine za binadamu. Hata hivyo wakati mwingine jamii hutumia haki za kitamaduni kama kisingizio cha kukandamiza wengine au kubinya haki zingine za binadamu katika jamii.