Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Somalia

Baadhi ya familia 280 walikimbilia kambi ya watu waliohama makazi yao huko Daniyle kusini mashariki mwa Somalia.
© UNICEF/Zerihun Sewunet

UN yahitaji dola bilioni 2.6 billion ili kusaidia watu milioni 7.6 Somalia 2023

Naibu mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu na mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Adam Abdelmoula, leo ametoa ombo maalum la dola bilioni 2.6 kwa ajili ya kuwasaidia mamilioni ya watu katika taifa hilo la Pembe ya Afrikaambako changamoto za mabadiliko ya tabianchi na mgogoro wa muda mrefu vimesababishaSomalia kuwa moja ya janga kubwa Zaidi la kibinadamu duniani.

Wanufaika wa miradi inayotekelezwa na FAO nchini Somalia
©FAO/Arete/Ismail Taxta

Uwekezaji wa kimkakati unahitajika ili kuboresha uhakika wa chakula na maji kwa mamilioni ya Wasomali

Wakati misaada ya kibinadamu imesaidia baadhi ya maeneo ya Somalia kutotumbukia kwenye baa la njaa, wananchi wa vijiji nchini humo bado wanaendelea kukabiliwa na ukosefu wa uhakika wa chakula limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO hii leo baada ya hivi karibuni kutangazwa matokeo ya uchunguzi wa uhakika wa chakula.