Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Wasichana wakibeba maji Yangambi nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC.
CIFOR/Axel Fassio

Pamoja na magumu wanayopitia, raia wa DRC waonesha mshikamano

Ikiwa leo ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibinadamu, OCHA inapatia nchi wanachama wa Umoja huo hali halisi ya kibinadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, , raia nchini humo licha ya machungu wanayopitia na madhila yanayowakabili  wameendelea kuonesha mshikamano wa ajabu baina yao ili angalau kupunguza machungu wakati jamii ya kimataifa ikihana kuwanusuru.

Sauti
2'32"
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu MONUSCO nchini DRC wakizungumza na wananchi wakazi wa jimbo la Kivu Kaskazini.
TANZBATT_8/Kapteni Tumaini Bagambo.

TANZBATT_7 yafunga virago DRC na kukabidhi kijiti kwa TANZBATT_8

Kikosi cha 7 cha Tanzania, TANZBATT_7 kwenye kikosi maalum cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO kimetamatisha jukumu lake rasmi na kukabidhi bendera kwa kikosi cha 8 au TANZBATT_8. Shuhuda wetu kutoka Beni, jimboni Kivu Kaskazini ni Luteni Issa Mwakalambo, afisa habari wa TANZBATT_7. 

Sauti
3'19"
Karatasi ya plastiki imetenganisha mama na mwanae atika kituo cha matibabu ya ebola Beni, Kivu Kasakzini nchini DRC.
© UNICEF/Thomas Nybo

Ebola DRC: UNICEF yachukua hatua kudhibiti kuenea 

Kufuatia serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kutangaza kifo cha mtu mmoja huko Butembo jimboni Kivu Kaskazini kutokana na ugonjwa wa Ebola, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limepeleka wafanyakazi zaidi na linajiandaa kupeleka vifaa vya matibabu.