Siku ya kimataifa ya waathirika wa matendo ya vurugu yanayotokana na dini au imani yaadhimishwa kwa mara ya kwanza.
Katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya kuadhimisha waathirika wa matendo ya vurugu yanayotokana na dini au imani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ulimwengu unapaswa kupinga na kukataa wale ambao kwa mabavu na kwa uongo wanashawishi kujenga imani potofu, kuchochea mgawanyiko na kueneza hofu na chuki.