Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

19 JUNI 2023

Leo jarida la Umoja wa Mataifa linaangazia siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili wa kingono katika mizozo ya vita, Umoja wa Mataifa umesema jinamizi hilo ni janga lililokita mizizi katika kukosekana kwa usawa, kanuni na tamaduni kali za masuala ya kijinsia.

Utasikia pia kuhusu maonesha ya athari ziletwazo na kauli za chuki ambapo wawakilishi watatu wa taasisi ya Kina mama wa Srebrenica walitembelea maonesho hayo na kuzungumzia maswahibu yaliyowakumba miaka 28 iliyopita na kuacha vidonda katika mioyo yao.

Sauti
14'13"

16 JUNI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia manufaa ya utumaji pesa kutoka nchi moja kwenda nyingine, na uwezeshaji wa wavuvi nchini Sudan Kusini. Makala tunakupeleka nchini Rwanda na mashinani nchini Colombia, kulikoni?  

Sauti
12'37"

15 JUNI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo inatupeleka Congo DRC kusikia kinachowasibu wakimbizi wa ndani waliofurishwa na waasi wa ADF na kinachofanywa na Umoja wa Mataifa kuwasaidia. Pia tunakuletea habari kwa ufupi za IOM, UNITAMS na WMO. Katika kujifunza lugha ya tunabisha hodi kwenye Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania BAKITA kufafanuliwa maana ya neno "KUYEYESA" 

Sauti
12'23"
UN News/Byobe Malenga

UNICEF: Idadi ya watoto waliotawanywa duniani imevunja rekodi na kufikia milioni 43.3

Katika kuelekea siku ya wakimbizi duniani itakayoadhimishwa wiki ijayo, ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF imeonya kwamba idadi inayoongezeka ya watoto kutawanywa duniani, inadhihirisha jinsi gani dunia ilivyoshindwa kushughulikia mizizi ya watu kutawanywa na kutoa suluhu ya muda mrefu hususan kwa watoto wanaolazimika kukimbia makwao.

Sauti
3'22"

14 JUNI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia watoto katika migogoro ya silaha na wale wanaokimbia makazi yao.  Makala tunakupeleka nchini Tanzania na mashinani tunasalia huko huko Tanzania, kulikoni? 

Sauti
15'24"

13 JUNI 2023

Hii leo ni Siku ya Kimataifa ya Uelewa Kuhusu Ualbino na kama ilivyo ada ya kila Jumanne tunakuletea mada kwa kina ambapo tutamsikia mwanamuziki Roben X akieleza kuhusu maisha yake ya Ualbino. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za DRC, Myanmar na Ukraine.  Mashinani tunasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa tukikuletea ujumbe kuhusu ujumuishaji na uajiri wa watu wenye ualbino.

Sauti
11'8"

08 JUNI 2023

Hii leo ni siku mada kwa kina na jaridani tunaangazia siku ya kimataifa ya bahari inayohimiza kuhakikisha bahari inakuwa safi na yenye afya ili iweze kuihudumia vyema jamii tutaangalia namna taka zinazotolewa baharini zinavyoweza kutumika kama malighafi bora ndani ya jamii. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo …. Na katika kujifunza kiswahili tunabisha hodi kwenye Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania BAKITA kufafanuliwa maana ya neno"RUWI", salía hapo hapo!

Sauti
11'20"

07 JUNI 2023

Jaridani hii leo tunaangazia siku za Umoja wa Mataifa na wawakimbizi wa Sudan wanaolelekea nchi jirani. Makala tunakupeleka nchini CAR na mashinani nchini Tanzania, kulikoni?

Sauti
12'5"