Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

31 AGOSTI 2020

Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO, leo limechapisha utafiti wake wa kwanza wa athari za janga la corona au COVID-19 kwa mifumo ya afya duniani, hali ikoje? Waathirika wa mafuriko makubwa yanayokumba maeneo mbalimbali ya Mashariki mwa Afrika na kusababisha athari  ikiwemo watu kupoteza kila kitu, hususan  nchini Kenya wamelishukuru shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa kuwasaidia.

Sauti
12'12"

28 AGOSTI 2020

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema janga la corona au COVID-19 limeanika wazi mifumo tete na pengo la usawa vitu ambavyo vinatishia msingi wa maendeleo endelevu, SDGs.  Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, limeendelea na juhudi zake za kusaidia kupambana na utapiamlo kwa watoto nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ingawa COVID-19 inatishia shughuli hizo znazolenga kuwaokoa watoto wapatao milioni 3.4. Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Michelle Bach

Sauti
11'46"

27 Agosti 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Flora Nducha

- Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF yasame Takribani theluthi ya watoto wa shule duniani kote, hawakuweza kupata masomo nje ya mazingira ya shule.

-Nini siri ya Mauritius kudhibiti COVID-19 katika muda mfupi

-Kutana na mkimbizi Khalili Ibrahim kutoka Syria ambaye ajali na athari za janga la corona au COVID-19 ilimlazimisha kumwachisha binti yake shule ili afanye kazi.

-Na kwenye makala leo  tunamulika safari ya Afrika kutokomeza ugonjwa wa Polio

Sauti
13'13"

26 Agosti 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Flora Nducha
- Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP lasema Mamilioni ya wakimbizi Afrika Mashariki wako njia panda baada ya mgao wa chakula kukatwa.
- Shirika la kijamii la ACAKORO limekuwa mkombozi mkubwa wa elimu kwa watoto masikini nchini Kenya baada ya shule kuendelea kufungwa kutokana na janga la corona au COVID-19.
- Mauritius, taifa la kisiwani lililo katika bahari ya Hindi limeelezea kile kilicholiwezesha kudhibiti ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 punde tu baada ya kuthibiti
Sauti
13'4"

25 Agosti 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Flora Nducha

-  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres  amesema COVID 19 imeathiri utalii na hivyo kuharibu ajira, uchumi na urithi wa asili

-  Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani, WFP yasaka dola milioni 235 kusambaza misaada ya chakula Lebanon kwa miezi 6 ijayo

Sauti
13'28"

24 Agosti 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Flora Nducha

-Wakulima wa Turkana wasema  Kama nzige hawa hawataisha na mvua ikanyesha japo kiasi, mifugo yetu itakufa.
wa Mataifa lipitishe azimio la kutambua siku hii mwaka 2018

-Mbio za Selous zachagiza uhifadhi wa mazingira na utalii endelevu Tanzania.

-Kutana na mtaalam wa huduma za kijamii za watoto nchini Cambodia Tim Sreyoun ambaye anasema licha ya janga la corona au COVID-19 ni wajibu wake kuhakikisha watoto wanahudumiwa na kulindwa dhidi ya ukatili kwani ni zahma aliyoipitia maishani mwake.

Sauti
13'20"

21 Agosti 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Flora Nducha
- Leo ni siku ya kukumbuka na kuenzi waathiriwa na manusura waugaidi, ikiwa ni maadhimisho ya tatu tangu Baraza Kuu la Umoja
Sauti
10'24"

20 Agosti 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Flora Nducha
- Mashirika ya Umoja wa Mataifa la afya duniani WHO na la kuhudumia watotoUNICEF zataka shule zifunguliwe kwa njia salama Afrika 
- Nzige vamizi wa jangwani wakiendelea kuharibu mazao kwenye kaunti ya Turkana nchini Kenya, shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa, FAO linaendelea na kampeni kubwa ili kupunguza tatizo la ukosefu wa chakula.
-Umoja wa Mataifa kupitia mashirika yake na wadau, wameendelea kutoa misaada kwa waathirika wa mlipuko uliotokea Agosti 4 katika mji mkuu wa
Sauti
13'12"

19 Agosti 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Flora Nducha

-Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibindamu na masula ya dharura OCHA yatoa shukrani zake kwa wahudumu wa kibinadamu kokote waliko katika kuokoa maisha.

- Ikiwa leo ni siku ya huduma za kibinadamu duniani Umoja wa Mataifa umesema unawaenzi wahudumu hao ambao wanakabiliana na changamoto lukuki katika kuokoa na kuboresha maisha ya mamilioni ya watu.

Sauti
13'27"

18 Agosti 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Flora Nducha
- Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema COVID-19 imeingilia na kuathiri huduma za ulinzi wa watoto katika nchi zaidi ya 100
-  Mkimbizi wa Syria asema "Nilichokiona Beirut sitosahau katu"  
-Machafuko yanayoendelea kushika kasi nchini Burkina Faso sasa yamewalazimisha zaidi ya watu milioni moja kufungasha virago na kuzikimbia nyumba zao kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na serikali limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.
Sauti
12'36"