FAO na ILO wasaka suluhisho la ajira za watoto hususan kwenye kilimo
Leo hii kote duniani mtoto 1 kati ya 10 anatumikishwa katika ajira ya watoto na wengi wao ni katika sekta ya kilimo limesema leo kongamano la kimataifa lililoandaliwa kwa njia ya mtandao na shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO kwa lengo la kusaka suluhu za kutokomeza ajira hiyo.
Flora Nducha na maelezo zaidi .
Hao ni baadhi ya watoto wakielezea ndoto zao na matamanio yao wengine wakitaka kuwa waalimu, wanamuziki, marubani na kadhalika, lakini sasa ndoto hizo zimeota mbawa baada ya kujikuta wamekwama katika ajira ya watoto.