Wanafunzi na wazazi wanufaika na mradi wa WFP wa chakula shuleni
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP nchini Rwanda, linaendesha programu ya chakula kutoka nyumbani kwenda shuleni, programu ambayo inatekeleza malengo 6 ya maendeleo endelevu, SDGs likiwemo namba 2 la kutokomeza njaa na hivyo kuwaacha wazazi na wanafunzi wakiwa na furaha. Leah Mushi ana taarifa zaidi.
(Taarifa ya Leah Mushi)
Programu ya kuwapatia wanafunzi mlo shuleni inatekelezwa katika nchi nyingi duniani na pengine huwa unajiuliza chakula hicho kinatoka wapi?