Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Benki ya Duniak/Simone D. McCourtie

Watunga sera chukueni hatua nchi zinufaike na TEHAMA- UNCTAD

Baadhi ya mataifa yanayoendelea yanaonesha uwezo wa kutumia na kuchukua teknolojia mpya ikilinganishwa na vipimo vya pato la kitaifa lakini nyingi bado zinasalia nyuma, imesema ripoti mpya ya Kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo, UNCTAD ya mwaka 2021 ambayo imetolewa leo Februari 25 mjini Geneva Uswisi.  Grace Kaneiya na maelezo zaidi.

Teknolojia hizo mpya ni zile ambazo zinatumia maendeleo ya dijitali na utandawazi ikiwemo akili bandia, mtandao wa kizazi cha sasa wa 5G uchapishaji kutumia bapa tatu au 3D, ndege zisizo na rubani na nyinginezo.  

Sauti
2'43"
UNHCR/Benjamin

Ingawa COVID-19 imesababishwa nikatwe miguu yangu, katu sitoacha kufuata ndoto yangu-

Kutana na binti kutoka Uganda, Christine Joyce ambaye anasema asilani hatolisahau janga la corona au COVID-19 ambalo mbali ya kumnyima masomo wakati wa sheria za kusalia majumbani limechangia kumwacha na kilema cha maisha. Hata hivyo amesema hatokata tamaa ya kutimiza ndoto yake ya kuendelea na masomo na hatimaye siku moja kuwa daktari.Jason Nyakundi na maelezo zaidi.

Christine Joyce mwenye umri wa miaka 15 ni mkazi wa Kampala nchini Uganda na sasa ana ulemavu wa kutokuwa na miguu yote miwili na anatumia kitimwendo. 

Audio Duration
2'28"
UN News/Assumpta Massoi

Kilimo hifadhi ndio mkombozi wetu- Wakulima Kigoma Tanzania

Kilimo hifadhi kinaturejesha ujana – Wanufaika Kigoma- TV

Nchini Tanzania mafunzo ya kilimo hifadhi yaliyotolewa mwaka jana na shirika la chakula na kilimo la Umoja wa MAtaifa, FAO kwa wakulima mkoani Kigoma yameanza kuzaa  matunda na wakulima ndio mashahidi. Assumpta Massoi na maelezo zaidi. 

Mkulima Merina Siganigwa mnufaika wa mafunzo ya kilimo hifadhi yaliyotolewa na FAO kwa wakulima wa kata ya Muzye wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma akitoa ushauri kwa mkulima jirani yake.

Sauti
2'16"
WFP/Carlos Alonzo

Wahamiaji Amerika ya Kati waathirika zaidi na njaa - WFP

Janga la njaa limeongezeka karibu mara nne katika miaka miwli iliyopita nchini El Salvador, Guatemala, Honduras na Nicaragua na kuwaacha takriban watu milioni 8 katika eneo hilo la Amerika ya Kati wakihitaji msaada mwaka huu wa 2021, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP.  Jason Nyakundi na maelezo zaidi.

Sauti
2'37"
UNICEF/Francis Emorut

Dola 1 iwekwezayo katika mlo shuleni huzalisha dola 9 - WFP

Mafanikio ya miongo kadha ya mgao wa chakula shuleni yaliyolenga watoto walio hatarini na wasio na uwezo wa kupata mlo bora, yako hatarini kutumbukia nyongo kutokana na janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19, imesema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa hii leo huko Roma Italia ikimulika hali ya mpango wa mlo shuleni duniai, SOSFW. Assumpta Massoi.

Sauti
2'46"
OCHA/Ivo Brandau

Jamii ya kimataifa ikihaha kunusuru DRC, jamii yashikamana kupunguza madhila

Ikiwa leo ofisi ya Umoja wa MAtaifa ya kuratibu misaada ya kibinadamu, OCHA inapatia nchi wanachama wa Umoja huo hali halisi ya kibinadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, , raia nchini humo licha ya machungu wanayopitia na madhila yanayowakabili  wameendelea kuonesha mshikamano wa ajabu baina yao ili angalau kupunguza machungu wakati jamii ya kimataifa ikihana kuwanusuru. Taarifa ya John Kibego inaeleza zaidi. 

Sauti
2'32"
UNICEF/Alessio Romenzi

Theluji pasi kifani yatishia maisha ya wakimbizi Lebanon

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema hali mbaya ya hewa inayoambatana na majira ya baridi kali  yaliyoghubikwa na kumwagika kwa theluji nyingi Mashariki ya Kati, imeongeza zahma kwa mamilioni ya wakimbizi na wakimbizi wa ndani kama inavyofafanua taarifa ya Jason Nyakundi 

Nchini Lebanon katika makazi yasiyo rasmi ya wakimbizi kwenye bonde la Beka theluji inamiminina pasi kifani, na kusababisha athari kwenye zaidi ya  asilimia 70 ya makazi haya kutokana na theluji kulundikana au mahema kuvuja. 

© UNICEF/UN0377403/Roger LeMoyne

Hali tete nyumbani Ituri, bora kusalia kambini- Mkimbizi Anasthasia

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kikongwe anayelea wajukuu wake baada ya mtoto wake kuuawa kwenye mapigano amekata tamaa ya maisha akisema hana matumaini yoyote na anahofia kuwa akirejea nyumbani atauawa. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.

Nyakati za asubuhi jimboni Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Anasthasia Chove mwenye umri wa miaka 72 akielekea shambani na wajukuu zake.

Baada ya kukwatua shamba lao sasa safari ya kurejea nyumbani wakiwa na mavuno ambayo ni mboga ya kabichi na mahindi.

UNDP Comoros/James Stapley

Mradi wa ILO Comoro wanusuru kilimo, barabara na kipato cha wananchi

Nchini Comoro, shirika la kazi duniani, ILO limetekeleza mradi wa kuinua maisha ya wakazi wa vijijini unaotoa fursa kwa wananchi kushiriki katika ajira zenye staha za ujenzi wa barabara na hivyo kufungua milango zaidi ya mauzo ya mazao yao ya kilimo na hatimaye kuondoa umaskini. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.

Mkoani Mboinkou katika kisiwa kikuu cha Comoro barani Afrika, wananchi wake kwa waume wakiwa katika ujenzi wa barabara, mradi wa kazi kwa ujira unaotekelezwa na ILO.