Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UNEP GRID Arendal/Peter Prokosch

Edwin Kinyanjui - Kutoka kuwa adui wa tembo hadi rafiki na mtetezi

Nchini Kenya kampeni ya kulinda wanyamapori nayoongozwa na shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP imezidi kupanua wigo wake ambapo hivi sasa hata watu ambao awali walikuwa adui wa wanyamapori, wamegeuka rafiki na walinzi wakuu wa wanyama hao kama njia mojawapo ya kuhifadhi misitu kama ile ya mlima  Kenya, bali pia bayonuai ambayo ni muhimu kwa viumbe vyote. Taarifa ya Anold Kayanda inaeleza zaidi.

Katikati ya msitu mnene kwenye miteremko ya mlima Kenya tunakutana na Edwin Kinyanjui, huyu ni askari wa wanyamapori katika Wakfu wa mlima Kenya. 

Sauti
2'20"
UNSMIL/Lason Athanasiadis

UNHCR mkombozi wa wakimbizi wajawazito wa Eritrea walioko Libya.

Kama sehemu ya huduma mbali mbali za ulinzi zinazotolewa kwa wakimbizi na wanaotafuta hifadhi nchini Libya, shirika la kuhudumia wakimbizi UNHCR kupitia mdau wake, Kamati ya kimataifa ya uokozi, IRC, wanatoa huduma za afya ya uzazi bila malipo kwa wanawake ambao ni wajawazito au wamejifungua hivi karibuni, na pia kuwapatia rufaa za kwenda kwenye vituo vikubwa zaidi kwa ajili ya kujifungua. Ahimidiwe Olotu na maelezo zaidi.

Sauti
2'13"
UNHCR/Martim Gray Pereira

Mashirika ya UN yahaha kunususu raia walioko katika hali tete Cabo Delgado.

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yameripoti kuwepo kwa mashambulizi dhidi ya raia kwenye mji wa Palma jimboni Cabo Delgado nchini Msumbiji na kusababisha maelfu ya watu kukimbilia maeneo ya jirani ikiwemo mpakani na Tanzania.

Mashirika hayo lile la uhamiaji, IOM, mpango wa chakula duniani , WFP,  ofisi ya kuratibu misaada ya dharura, OCHA na lile la kuhudumia wakimbizi, UNHCR,  yamesema makumi kadhaa ya watu wameuawa wakati wa mashambulio hayo kutoka kwa waasi waliojihami ambao yaripotiwa waliingia mjini humo mwishoni mwa wiki. 

Sauti
2'31"
Alhagie Manka/ UNFPA Gambia

Mjasiriamali Fatou: Msaada wa IFAD umeniokoa mimi na familia yangu.

Duniani kote mamilioni ya wasichana na wanawake vijijini wanaweza kuendesha maisha yao kwa kutumia ardhi inayowazunguka, lakini mara nyingi wanashindwa kufanya hivyo kwa ukosefu wa mtaji wa kuanzia kutekeleza malengo yao, Sasa mfuko wa kimataifa wa maendeleo ya kilimo IFAD unashirikiana na serikali mbalimbali kutoa mitaji inayowawezesha wasichana kuingia katika bishara ya kilimo kama  alivyofanya Fatou Secan nchini Gambia. Taarifa ya Flora Nducha inaeleza zaidi.

Sauti
2'3"
© UNICEF/Juan Haro

Ndoto ya mtoto mkimbizi kuwa daktari yawezeshwa na UNICEF.

Nchini Niger watoto wakimbizi waliolazimika kukimbia Libya kutokana na ghasia za ugenini hivi sasa wanaona nuru ya maisha yao baada ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNICEF, kuwapatia maeneo salama siyo tu ya kucheza bali pia kujifunza.  Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Miongoni mwa watoto hao ni Wichah Nasradine, mtoto mwenye uraia wa Sudan, akiwa Agedez nchini Niger, na ana umri wa miaka 13. 

Sauti
2'
UN Photo/Antonio Fiorente

UN yamenzi Rais John Magufuli kwa kupeperusha bendera nusu mlingoti

Hii leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, bendera ya Umoja wa Mataifa inapepea kwa nusu mlingoti kuashiria maombolezo ya kifo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli aliyefariki dunia tarehe 17 mwezi huu wa Machi.

Rais Magufuli aliaga dunia jijini Dar es salaam naamezikwa leo nyumbani kwake huko Chato mkoani Geita nchini Tanzania.

Sauti
1'53"
UNHCR

Tafadhali Kenya msifunge makambi ya wakimbizi Dadaab na Kakuma bila suluhu:UNHCR

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limeisihi serikali ya Kenya kuhakikisha kwamba maamuzi yoyote itakayofanya kuhusu kambi za wakimbizi zilizoko nchini humo yanakuwa ni suluhu endelevu kwa wakimbizi hao. Flora Nducha na taarifa zaidi

(TAARIFA YA FLORA NDUCHA)

Rai hiyo ya UNHCR iliyotolewa kupitia ukurasa wake wa Twitter Jumatano jioni imekuja baada ya serikali ya Kenya kutoa taarifa ya kuelezea nia yake ya kutaka kuzifunga kambi za wakimbizi za Dadaab na Kakuma zilizoko nchini humo. 

Sauti
2'23"
© FAO/Petterik Wiggers

Muhogo mkombozi umetukomboa kweli Kigoma: Wakulima

Nchini Tanzania harakati za Umoja wa Mataifa kujengea uwezo wakulima katika kutambua mbinu bora za kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi, zimezaa matunda huko mkoani Kigoma baada ya wakulima wa wilayani Kakonko kuvuna zao la muhogo walilopanda kwa kuzingatia ushauri wa wataalamu. Taarifa ya Ahmidiwe Olottu anatupasha zaidi

(TAARIFA YA AHIMIDIWE OLOTTU)

Sauti
3'7"
UN Photo/Devra Berkowitz

Tuwaenzi waathirika wa utumwa kwa kutokomeza misingi yake inayoendelea leo hii:UN

Katika siku ya kimataifa ya kuwakumbuka waathirika wa utumwa na biashata ya utumwa katika bahari ya Atlantiki hii leo Katiku Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema ili kuwaenzi vyema mamilioni ya watu wenye asili ya Afrika waliopitia madhila asiyoelezeka katika utumwa na biashara ya utumwa ni vyema kuyania wazi yaliyowasibu na kuhakikisha yatokomezwa.

Katika ujumbe wake wa siku hii Antonio Guterres amesema

(SAUTI YA ANTONIO GUTERRES)

Sauti
1'38"