Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mapigano ya kikabila Sudan Kusini yachochea hali ngumu- Lacroix

Mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani kwenye Umoja wa Mataifa Jean-Pierre Lacroix akizungumza kuhusu uslama nchini Sudan Kusini. Picha: UM/Manuel Elias

Mapigano ya kikabila Sudan Kusini yachochea hali ngumu- Lacroix

Gharama ya mzozo wa Sudan Kusini kwa wananchi inazidi kuongezeka kila uchao wakati huu ambapo mapigano yanaendeleo huku mahitaij ya kibinadamu nayo yakiongezeka.

Mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani kwenye Umoja wa Mataifa Jean-Pierre Lacroix amesema hayo hii leo akiwasilisha ripoti ya siku 90 ya Katibu Mkuu wa umoja huo kuhusu hali ya usalama na kibinadamu nchini Sudan Kusini.

image
Wakimbizi wa ndani wajengewa makazi ya muda baada ya kutawanywa na machafuko nchini Sudan Kusini. Picha: UNHCR
Bwana Lacroix amesema hadi sasa watu milioni 4 wamepoteza makazi yao tangu mapigano yaanze nchini humo mwaka 2013 huku ukiukwaji wa haki za binadamu ikiwemo uporaji, uchomaji wa nyumba na ukatili wa kingono vikishamiri.

(Sauti ya Jean-Pierre Lacroix)

Kinachoongeza zaidi athari kwenye usalama ni mapigano ya kikabila. Mfano wa pekee zaidi ni tarehe 28 mwezi novemba ambapo watu wapatao 45 waliuawa, 19 walijeruhiwa na mamia waliona nyumba zao zikitekezwa kwa moto wakati kikundi cha Murle waliposhambulia kijiji cha wadinka huko Jonglei.”

Bwana Lacroix hata hivyo akagusia pia mjadala wa kitaifa unaofanyika Sudan Kusini kuchambua vyanzo vya mzozo akisema..

(Sauti ya Jean-Pierre Lacroix)

“Kwa maelezo mengi, mashauriano hayo yamekuwa ya dhati na yameibua hofu sahihi kabisa za umma kuhusiana na uongozi, rushwa na utawala wa kisheria. Hata hivyo wasiwasi uliopo ni kwa jinsi gani matokeo yake yatatumika »

image
Walinda amani wa UNMISS wapiga doria Jonglei nchini Sudan Kusini huku wakiangalia usalama wa watoa misaada. Picha: UM/Tim McKulka
Hatimaye akataja mambo matano ya kuzingatiwa ili kuleta nuru Sudan Kusini ambayo ni pamoja na kuzingatia haraka sitisho la mapigano kwa pande zote kwenye mzozo, kushughulikia changamoto za watoa misaada katika kusambaza huduma hizo na kuondoa vikwazo dhidi ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa Sudan Kusini, UNMISS.