Shirika la chakula na kilimo FAO na shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM leo wametia saini makubaliano mapya ya ushirika kuhusu suala la uhamiaji na kundi la kimataifa la uhamiaji GMG.
Nchini Sudan Kusini asilimia 30 ya mifugo iko hatarini kutokana na ukosefu wa chanjo dhidi ya magonjwa hatari, limesema shirika la chakula na kilimo duniani, FAO. Flora Nducha na maelezo zaidi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali mauaji ya waandamanaji huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akisema kitendo hicho hakikubaliki.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali mauaji ya waandamanaji huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akisema kitendo hicho hakikubaliki.
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC watu sita wameuawa jumapili kwenye mji mkuu Kinshasa wakati wa maandamano yaliyoandaliwa na kanisa katoliki nchini humo. John Kibego na ripoti kamili.
Umoja wa Mataifa umesema uko tayari kusaidia nchi za Asia ya Kati zinapoimarisha ushirikiano baina yao na Afghanistan ili kufanikisha malengo ya amani, maendeleo endelevu, utulivu na usalama.